Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Askofu Bagonza: Niko salama, nitawashtaki kwa Mungu
Habari MchanganyikoTangulizi

Askofu Bagonza: Niko salama, nitawashtaki kwa Mungu

Askofu Benson Kagonza, KKKT Dayosisi ya Karagwe
Spread the love

ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe mkoani Kagera amesema, “mimi niko salama, naendelea na majukumu yangu kama kawaida. Mimi si mtumishi wa umma, nitawashtaki kwa Mungu.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kiongozi huyo wa kiroho, amesema maneno hayo leo Jumamosi tarehe 12 Desemba 2020 alipozungumza na MwanaHALISI Online lililotaka kujua maendeleo yake hasa baada ya uwepo wa taarifa za kutishiwa usalama wake.

Amesema, kama wiki moja iliyopita alipokea taarifa za kutishiwa, akaendelea kukaa kimya.

“Vilianza kama vituko, watu kunitumia ujumbe wa kunitishia kuwa mimi ni mpinzani, napinga serikali, ngoja nitaona, kama unafikiri mimi ni mjanja utaona, kichwa changu kitakapotenganishwa.”

“Baadaye nikapigiwa simu na watu wema, waliokatika nafasi nyeti na kuniambia niwe mwangalifu kuwa hawa watu wamepiga kambi Karagwe maaluum kwa kukushughulikiwa wewe kama walivyomfanya askafu mwenzako,” amesema Askofu Bagonza.

Amesema “siamini kwamba serikali inaweza kutuma watu wajinga namna hiyo, mimi niko salama. Niko salama na hatua zote za kuimalisha ulinzi wangu ziko vizuri.”

Askofu Bagonza amesema “naendelea kutoa huduma na hakuna jambo lolote baya nililofanya. Najifahamu tangu nikiwa mdogo, kitu pekee ninachokithamini ni uhuru wa maoni. Situkani mtu na wala sifanyi kosa.”

Akijibu kuwa amekwisha kutoa taarifa polisi, Askofu Bagonza amesema “ukiona hao watu wema walionipigia kama ni polisi sasa nakwenda kuripoti nini polisi? Ukionewa na polisi utampeleka polisi? Ikiwa watu wema walionipigia wanaweza kuwa polisi baadhi yao, sasa nakwenda kufanya nini? Mimi si mtumishi wa umma, nitawashtaki kwa Mungu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Ditopile aungana na Wana-Kongwa kwa Iftar, wamuombea dua Rais Samia

Spread the loveKATIKA muendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Mbunge wa Viti...

Habari Mchanganyiko

PSSSF yawekeza kwenye viwanda 4, kuzalisha ajira 3,000

Spread the loveKATIKA kuisaidia Serikali kupunguza tatizo la uhaba wa ajira nchini,...

Habari Mchanganyiko

Luhemeja ahimiza utunzaji rasilimali maji kwa faida ya vizazi vijavyo

Spread the love  NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Cyprian Luhemeja...

Habari Mchanganyiko

NSSF yawapa darasa wahariri uwekezaji wa nyumba, yapewa cheti

Spread the loveMFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetoa wito...

error: Content is protected !!