Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu ashauri Bajeti Kuu iinue kipato cha Watanzania
Habari Mchanganyiko

Askofu ashauri Bajeti Kuu iinue kipato cha Watanzania

Spread the love

IKIWA imebaki siku moja Serikali kuwasilisha Bajeti Kuu bungeni, Askofu wa Kanda ya kati wa makanisa la Baptist, Antony Mlyashimba ameitaka ametoa wito kwa Serikali kuhakikisha bajeti hiyo inalenga kuinua kipato cha Watanzania. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma (endelea).

Pia ametoa wito kwa serikali kupunguza matumizi ya anasa kama vile kununua magari ya bei ghali, kupunguza misafara ya viongozi wa kuu wa serikali na hata safari za nje ili kubana maumizi.

Askofu Mlyashimba ametoa wito huo jana tarehe 12 Juni, 2022 muda mfupi baada ya kumaliza kuhudumia ibada maalum ya shukrani na kushiriki meza ya Bwana katika kanisa hilo.

Aidha, ameishauri serikal kuwekeza zaidi katika masuala ya uzalishaji katika sekta za kilimo, afya, elimu pamoja na mifugo.

Kiongozi huyo wa kiroho amesema serikali inatakiwa kuwa na vipaumbele vichache lakini vinavyotekelezeka badala ya kuwa na vipaumbele vingi ambavyo havitekelezeki.

“Pia serikali itoe ruzuku katika sekta ya kilimo ili kukuza uzalishaji.

“Kuna kila sababu ya kuhakikisha Tanzania inaruhusu uwepo wa uraia pacha jambo ambalo litasaidia kukuza uchumi na kuwafanya watu waliopo nchi za nje kurudi na kuwekeza ndani,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!