Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Askari mwingine wa Tanzania afariki DR Congo
Habari Mchanganyiko

Askari mwingine wa Tanzania afariki DR Congo

Spread the love

WALINDA amani saba wa Umoja wa Mataifa akiwemo Mtanzania mmoja na wanajeshi sita wa Malawi wamepoteza maisha katika operesheni ya pamoja iliyofanywa na kikosi chake na Jeshi la DR Congo dhidi ya kundi la waasi la ADF. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, tukio hilo limetokea hivi karibuni katika mji wa Beni Kaskazini mwa Kivu, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo hadi sasa hakuna kundi lililobainika kutekeleza shambulio hilo.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa, kuna walinda amani kadhaa kutoka Jeshi la Congo pia wameripotiwa kuuawa au kujeruhiwa wakati askari kumi wakijeruhiwa huku mmoja akipotea kusikojulikana.

Dujarric amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ametuma salamu za rambi rambi kwa familia za walinda amani waliopoteza maisha, na kuvitaka vikundi vinavyotekeleza mapigano kusitisha kwani mapigano hayo yanaleta ugumu katika kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Mji wa Beni ulioko Kaskazini mwa Kivu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ni eneo lililoathiriwa zaidi na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Chanzo: BBC Swahili

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!