WALINDA amani saba wa Umoja wa Mataifa akiwemo Mtanzania mmoja na wanajeshi sita wa Malawi wamepoteza maisha katika operesheni ya pamoja iliyofanywa na kikosi chake na Jeshi la DR Congo dhidi ya kundi la waasi la ADF. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).
Kwa mujibu wa Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, tukio hilo limetokea hivi karibuni katika mji wa Beni Kaskazini mwa Kivu, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo hadi sasa hakuna kundi lililobainika kutekeleza shambulio hilo.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa, kuna walinda amani kadhaa kutoka Jeshi la Congo pia wameripotiwa kuuawa au kujeruhiwa wakati askari kumi wakijeruhiwa huku mmoja akipotea kusikojulikana.
Dujarric amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ametuma salamu za rambi rambi kwa familia za walinda amani waliopoteza maisha, na kuvitaka vikundi vinavyotekeleza mapigano kusitisha kwani mapigano hayo yanaleta ugumu katika kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Mji wa Beni ulioko Kaskazini mwa Kivu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ni eneo lililoathiriwa zaidi na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Chanzo: BBC Swahili
Leave a comment