Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askari mwingine wa Tanzania afariki DR Congo
Habari Mchanganyiko

Askari mwingine wa Tanzania afariki DR Congo

Spread the love

WALINDA amani saba wa Umoja wa Mataifa akiwemo Mtanzania mmoja na wanajeshi sita wa Malawi wamepoteza maisha katika operesheni ya pamoja iliyofanywa na kikosi chake na Jeshi la DR Congo dhidi ya kundi la waasi la ADF. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, tukio hilo limetokea hivi karibuni katika mji wa Beni Kaskazini mwa Kivu, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo hadi sasa hakuna kundi lililobainika kutekeleza shambulio hilo.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa, kuna walinda amani kadhaa kutoka Jeshi la Congo pia wameripotiwa kuuawa au kujeruhiwa wakati askari kumi wakijeruhiwa huku mmoja akipotea kusikojulikana.

Dujarric amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ametuma salamu za rambi rambi kwa familia za walinda amani waliopoteza maisha, na kuvitaka vikundi vinavyotekeleza mapigano kusitisha kwani mapigano hayo yanaleta ugumu katika kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Mji wa Beni ulioko Kaskazini mwa Kivu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ni eneo lililoathiriwa zaidi na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Chanzo: BBC Swahili

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!