Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Asilimia 75 Dodoma wana uoni hafifu, trakoma! ushirikina watajwa
Habari Mchanganyiko

Asilimia 75 Dodoma wana uoni hafifu, trakoma! ushirikina watajwa

Mgonjwa wa macho akipata vipimo
Spread the love

 

ASILIMIA 75 hadi 85 ya wakazi wa jiji la Dodoma wanakabiliwa na matatizo mbalimbali ya macho ikiwamo uoni hafifu pamoja na ugonjwa wa trakoma unaonezwa zaidi na inzi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma .. (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 18 Oktoba mwaka huu na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Macho kutoka katika Hospitali ya Rufaa Dodoma, Dk. Msigalo Erasto wakati akielezea hali ya magonjwa mbalimbali ya macho katika maadhimisho ya wiki ya afya ya macho duniani.

Dk. Erasto amesema mojawapo ya chanzo cha tatizo la uoni hafifu ni matumizi ya simu kwa muda mrefu hususani mwanga wa simu hizo za mkononi, kuangalia televisheni na kompyuta kwa muda mrefu.

Amesema watu wengi wanatatizo la afya ya macho kutokana na mwamko mdogo wa watu kupima afya ya macho mara kwa mara.

Akizungumzia kuhusu Mkoa wa Dodoma, Dk. Erasto amesema wagonjwa wengi wamekuwa wakihusisha matatizo ya macho na imani za kishirikina.

“Tumeona kuwa mkoa wa Dodoma una wagonjwa wengi wa macho na kibaya zaidi wamekuwa wakihusisha ugonjwa wa macho na imani za kishirikina.

“Tunapenda kuhimiza jamii kujitokeza na kujenga desturi ya kupima afya ya macho ili kuhakikisha wanapata matibabu kwa wakati pale wanapogundulika kuwa wanatatizo.

“Katika wiki hii ya maadhimisho ya afya ya macho duniani tunafanya upimaji wa huduma ya macho bure hivyo tunahamasisha jamii kuona umuhimu wa upimaji wa macho na inapotokea tatizo wapatiwa matibabu” ameeleza Dk. Erasto.

Aidha, baadhi ya wananchi wamesema wanakosa huduma hiyo kutokana na vituo vya afya kuwa mbali.

“Elimu ya upimaji wa afya ya macho bado haijaeleweka kwa watu wengi lakini pia huduma zinapatikana kwa tabu, tunachoomba ni serikali kusogeza huduma hiyo karibu na jamii” amesema mmoja wa wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!