Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Aprili Mosi siku ngumu kwa Halima Mdee
Habari za Siasa

Aprili Mosi siku ngumu kwa Halima Mdee

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe akiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

APRILI Mosi mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam itaamua kama Halima Mdee, Mbunge wa Kawe ana kesi ya kujibu ama la! Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Mdee anadaiwa tarehe 3 Julai 2017, katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alitoa alitoa lugha ya matusi dhidi ya  Rais John Magufuli.

Alitamka kwamba ‘anaongea hovyo, anatakiwa afungwe breki,’ kitendo kinachodaiwa kuwa ni udhalilishaji kwa Rais Magufuli na kwamba, kauli hiyo ingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Leo tarehe 20 Februari 2020, mbele ya Hakim Mkazi Mkuu Thomas Simba, wakili wa serikali mwandamizi Wankyo Simon amedai, upande wa mashitaka umefunga ushahidi wa mashahidi watatu katika kesi hiyo.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Aprili Mosi 2020, kwa ajili ya kutoa uamuzi kama Mdee ana kesi ya kujibu ama la.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!