Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Apigwa risasi akiamulia ugomvi wa mke na mume
Habari Mchanganyiko

Apigwa risasi akiamulia ugomvi wa mke na mume

Spread the love

 

JESHI la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, linamshikilia mfanyabiashara Issack Ngowi (29), kwa tuhuma za kumjeruhi kwa risasi Bakari Stambuli (40), aliyekuwa anaamua ugomvi kati yake na mkewe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumapili, tarehe 2 Januari 2022 na Kamanda wa Jeshi la Polisi Kilimanjaro, ACP Simon Marwa Maigwa, akitoa taarifa ya hali ya usalama ya mkoa huo, katika kipindi cha siku kuu ya mwaka mpya.

Taarifa ya Kamanda Maigwa imesema kuwa, tukio hilo lilitokea usiku wa tarehe 31 Desemba mwaka jana, maeneo ya Mjorohoroni, Moshi Manispaa mkoani humo, ambapo mtuhumiwa alimpiga risasi mhanga eneo la bega la mkono wa kushoto.

“Eneo la tukio kumepatikana ganda moja la risasi na bastola, mtuhumiwa anamiliki risasi hiyo kihalali.  Baada ya tukio alikimbia na kuacha silaha,  tayari amekamatwa.Chanzo cha tukio hilo ni mgogoro ulioibuka kati ya mtuhumiwa na mke wake, uliopelekea mhanga kuingilia kati kwa lengo la kuamulia,” imesema taarifa ya Kamanda Maigwa.

Taarifa ya Kamanda Maigwa imesema, mhanga wa tukio hilo ametibiwa katika Hospitali ya Mawezi, mkoani Kilimanjaro na kuruhusiwa, kwa  sasa anaendelea na matibabu akiwa nyumbani.

“Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya taratibu za kiupelelezi kukamilika. Jeshi la Polisi Kilimanjaro linatoa rai kwa wananchi wanaomiliki silaha kihalali,  halitasita kuwanyang’anya wale wote wanaotumia silaha hizo kinyume na taratibu na matakwa ya kisheria,” imesema taarifa ya Kamanda Maigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!