WAISLAM wa Madhuhebu ya Answer Sunna nchi wameungana na Waislamu wengine duniani katika kusherehekea Sikukuu ya Eid Alhaji. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Katiba ibada ya Swala ya Eid iliyofanyika leo kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam, mtoa mawaidha baada ya swala hiyo Sheikh Jadu Mcheni amesema, jambo kubwa na ushindi kwa Waislam ni umoja.
Shikh Mcheni amesema kuwa, Waislam watakapokuwa na umoja, hakuna jambo linaloweza kuwayumbisha kutokana na msikamano ulio imara.
Pia ametoa ujumbe wa kushikamana na ibada ya sadaka ambapo ni miongoni mwa mambo muhimu yanayotakatisha vitendo vya muumini mbele ya Mola wake.
“Tunapaswa kukumbuka kutoa sadaka endelezu, huku ndio kupona kwetu mbele ya Allah. Miongoni mwa sadaka tunazotakiwa kuzikimbilia ni kama ujenzi wa nyuma za ibada ama kutoa Waqf,” amesema.
Sheikh Mcheni ameuelezea umma uliofurika kwenye swala hiyo kuwa, pamaoja na mapito ya sasa Waislam wanapaswa kusaidiana.
Ibada ya swala ya Eid leo tarehe 21 Agosti 2018 imeyofanyika baada ya Waislam waliokwenda Hijja, Makka kusimama kisimamo cha Arafa jana Jumatatu na kutekeleza Ibada ya Kuchinja leo Jumanne.
Miongozi mwa nchi za Afrika zilizoswali Swala ya Eid kitaifa ni pamoja na Kenya, Uganda, Burundi, Jamhuri ya Kidemoksia ya Kongo (DRC) na Zambia.
Leave a comment