Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Angola, Rwanda, DRC, Rwanda, Kenya zanufaika chanzo ya corona
Kimataifa

Angola, Rwanda, DRC, Rwanda, Kenya zanufaika chanzo ya corona

Spread the love

 

NCHI kadhaa Afrika ikiwa ni pamoja na Rwanda, Kenya, Uganda, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), tayari zimepokea chanjo ya virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Chanjo hiyo aina ya AstraZeneca tayari imesambazwa kwenye mataifa hayo, ambapo Kenya imepokea jumla ya dozi milioni 1.02.

Katika mgao wa chanjo hiyo, DRC imepokea dozi milioni 1.7 kati ya dozi mil 6.9 za chanjo hiyo usiku wa jumanne tarehe 2 Machi 2021. chanzo hiyo imepokewa na Waziri wa afya wa nchi hiyo, Eteni Longondo.

Angola imepokea jumla ya dozi 624,000 huku Gambia ikiwa imepokea dozi 36,000 leo Jumatano tarehe 3 Machi 2021.

Pia leo Jumatano asubuhi, Rwanda imepokea dozi yake ya kwanza ya chanjo ya Oxford-AstraZeneca huku ikitarajia dozi 102,960 za chanjo ya Pfizer, kulingana na Wizara ya Afya ya nchi hiyo.

Rwanda inatarajia kupokea jumla ya chanjo 1,098,960 za AstraZeneca na Pfizer, katika mpango wa Covax unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa (UN). katika mpango wa chanjo hiyo, Tanzania haimo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!