KUELEKEA kwenye mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu kwa kombe la mataifa Afrika dhidi ya Uganda, kocha mjuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Emanuel Amunike amewajia juu wale wote wanaobeza aina ya mfumo wa uchezaji anao utumia ndani ya kikosi hicho bila kuangalia sifa za wachezaji. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)
Kocha huyo amezungumza hayo mbele ya waandishi wa habari kuelekea mchezo wa kesho na kusema kuwa muda mwengine mfumo sio shida, bali sifa za wachezaji watakaoweza kuendana na mfumo huo ndio muhimu.
“Watu wengi wanaongelea kuhusu mifumo kwa Mfano (3-5-2) (4-1-4-1) muda mwingine kuwa na wachezaji wenye sifa inayoendana na mifumo hiyo ndio muhimu zaidi” alisema Emmanuel Amunike
Hali hiyo ilitokea baada ya Tanzania kufungwa katika mchezo wa kundi L dhidi ya Lesotho kwa bao 2-0 na lawama zote kumuangukia yeye ambaye ndio mkuu wa benchi la ufundi kwa kushindwa kuipanga timu yake vizuri.
Katika kuelekea mchezo dhidi ya Uganda Amunike alisema kuwa kuwa katika mchezo wa kesho hautakuwa mwepesi kwa kuwa Uganda hawajaja hapa kulala ingawa wameshakata tiketi ya kushiriki michuano hiyo June, 2019 nchini Misri.
Tanzania inahitaji ushindi wa hali na mali katika mchezo huo ili iwese kufanikiwa kufuzu kwa michuano hiyo baada ya kupita miaka 39 toka mara ya mwisho ilipo shiriki michuano hiyo 1980 nchini Nigeria.
Leave a comment