Friday , 9 June 2023
Home Kitengo Michezo Amunike amtosa Kichuya, awarudisha nyota wa Simba
Michezo

Amunike amtosa Kichuya, awarudisha nyota wa Simba

Spread the love

KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania, Emmanuel Amunike ametangaza majina ya wachezaji 30 watakaoingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na mchezo dhidi ya Cape Verde, huku jina la kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba Shiza Kichuya likikosekana kwenye orodha hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kukosekana jina la mchezaji huyo katika kikosi kilichotangazwa na Amunike pengine kinaweza kutafsiriwa kuwa kiwango chake kimeshuka kwa siku za hivi karibuni katika klabu yake ya Simba hivyo kutopata nafasi ndani ya Stars.

Mchezo huo wa Tanzania na Cape Verde unatarajiwa kuchezwa 12 Oktoba, 2018 na siku nne baadae watarudiana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Wachezaji walioitwa kwenye kikosi hicho ni sambamba na walinda mlango, Aishi Manula, Beno Kakolanya, Mohamed Abdulahman, huku walinzi wakiwa ni Hassan Kessy (Nkana), Shomari Kapombe (Simba), Salum Kimenya (Prisons), Gadiel Michael (Yanga), Paulo Ngalema, Ally Sonso (Lipuli), Aggrey Morris, David Mwantika, Abdallah Kheri (Azam), Kelin Yondani, Andre Vicent (Yanga) na Abdi Banda (Baroka).

Viungo wapo Himid Mao (Petrojet), Saimon Msuva (El Jadida), Mudathir Yahya, Frank Domayo (Azam), Jonas Mkude (Simba), Feisal Salum (Yanga), Salum Kihimbwa (Mtibwa Sugar) na Farid Musa (Tenerife).

Huku washambuliaji ni Mbwana Samatta (KRC Genk), Thomas Ulimwemgu (Al Hilal), John Bocco (Simba), Yahya Zayd (Azam), Kelvin Sabato (Mtibwa Sugar), Rashid Mandawa (BDF XI) na Shaban Chilunda (Tenerife).

Stars ambao mpaka sasa wana alama mbili baada ya kwenda sare katika michezo miwili ya awali inahitaji kushinda mchezo huo ili iweze kujitengenezea nafasi nzuri ya kufuzu kwa mara ya pili katika michuano hiyo ya kombe la mataifa Afrika AFCON.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariMichezo

Benki ya NBC yazindua kombe jipya la Ligi Kuu Tanzania Bara

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa Ligi ya NBC , Benki ya Taifa...

MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Samia aipongeza klabu ya Yanga kwa hatua iliyofikia

Spread the love RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Yanga waitwa Ikulu kesho Jumatatu

Spread the love RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kesho Jumatatu, tarehe...

error: Content is protected !!