Fortunat Biselele, aliyekuwa msaidizi wa Rais Felix Tshisekedi wa Kongo DRC, amepelekwa katika Gereza Kuu la Makala jijini Kinshasa, baada ya malumbano ya saa sita na viongozi wa mashtaka. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Taarifa zinasema, Biselele, aliyekuwa msaidizi binafsi wa Rais Tshisekedi, alipelekwa katika Gereza hilo Ijumaa usiku tarehe 20 Januari, 2023.
Vipande vya video vimemuonesha Biselele, akisindikizwa wanajeshi kwenda katika Ofisi ya kiongozi wa mashtaka. Baadaye usiku, alionekana akiwa anasindikzwa na polisi kwenda Gerezani.
Biselele, aliondolewa kwenye Baraza la Mawaziri tarehe 14 Januari 2023,na kuzuiwa, lakini mpaka sasa hakuna sababu rasmi iliyotolewa kuhusu kukamatwa na kusimamishwa kwake kazi.
Hata hivyo, ripoti kutoka kwenye jarida la Africa Intelligence,inaeleza mshauri huyo wa zamani wa rais Tshisekedi, alikuwa anashukiwa kushirikiana na serikali ya Rais Paul Kagame nchini Rwanda.
Inaripotiwa kuwa, mwanzano mwa utawala wa Rais Tshisekedi, alijaribu kumleta karibu na Rais Kagame.
Uhusiano kati ya Kigali na Kinshasa, umeyumba, kufuatia madai ya DRC kuwa Rwanda, inawaunga mkono waasi wa M 23, shutuma ambazo rais Kagame, ameendelea kukanusha.
Leave a comment