Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Aliyekuwa msaidizi wa Rais DRC apelekwa gerezani
Kimataifa

Aliyekuwa msaidizi wa Rais DRC apelekwa gerezani

Spread the love

Fortunat Biselele, aliyekuwa msaidizi wa Rais Felix Tshisekedi wa Kongo DRC, amepelekwa katika Gereza Kuu la Makala jijini Kinshasa, baada ya malumbano ya saa sita na viongozi wa mashtaka. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Taarifa zinasema, Biselele, aliyekuwa msaidizi binafsi wa Rais Tshisekedi, alipelekwa katika Gereza hilo Ijumaa usiku tarehe 20 Januari, 2023.

Vipande vya video vimemuonesha Biselele, akisindikizwa wanajeshi kwenda katika Ofisi ya kiongozi wa mashtaka. Baadaye usiku, alionekana akiwa anasindikzwa na polisi kwenda Gerezani.

Biselele, aliondolewa kwenye Baraza la Mawaziri tarehe 14 Januari 2023,na kuzuiwa, lakini mpaka sasa hakuna sababu rasmi iliyotolewa kuhusu kukamatwa na kusimamishwa kwake kazi.

Hata hivyo, ripoti kutoka kwenye jarida la Africa Intelligence,inaeleza mshauri huyo wa zamani wa rais Tshisekedi, alikuwa anashukiwa kushirikiana na serikali ya Rais Paul Kagame nchini Rwanda.

Inaripotiwa kuwa, mwanzano mwa utawala wa Rais Tshisekedi, alijaribu kumleta karibu na Rais Kagame.

Uhusiano kati ya Kigali na Kinshasa, umeyumba, kufuatia madai ya DRC kuwa Rwanda, inawaunga mkono waasi wa M 23, shutuma ambazo rais Kagame, ameendelea kukanusha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

error: Content is protected !!