MTU mchafu zaidi duniani Amou Haji aliyekaa zaidi ya miaka 50 bila kuoga amefariki duniani miezi michache baada ya kuogeshwa kwa lazima. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Haji alikuwa amekataa kutumia sabuni na maji kwa zaidi ya nusu karne, akihofia ingemfanya kuwa mgonjwa.
Raia huyo wa Iran , ambaye aliishi katika jimbo la kusini la Fars, aliepuka majaribio ya hapo awali ya wanakijiji kutaka kumsafisha.
Lakini, kulingana na vyombo vya habari vya ndani, Haji hatimaye alikubali shinikizo na kuoga miezi michache iliyopita.
Kwa mujibu wa shirika la habari la IRNA la Iran, aliugua muda mfupi baadaye na kufariki siku ya Jumapili.
Katika mahojiano ya awali, yaliyotolewa na gazeti la Tehran Times mwaka 2014, Haji alifichua chakula anachopenda zaidi ni nungu, na kwamba aliishi kati ya shimo ardhini na kibanda cha matofali kilichojengwa na wakaazi wa kijiji cha Dejgah.
Aliiambia kituo hicho kwamba uamuzi wake ulitokana na vikwazo vya kihisia wakati alipokuwa mtoto mdogo.
Kutooga kwa miaka mingi kulimwacha akiwa ngozi yake imezibwa na tope na usaa, IRNA ilisema, huku chakula chake kikiwa nyama iliooza na maji chafu .
Haji hakujulikana kuwa na familia , lakini wanakijiji walijaribu kumuangalia.
Pia alikuwa akipenda kuvuta sigara, akipigwa picha angalau mara moja akivuta sigara zaidi ya mara moja.
Jaribio la kumuogesha, au kumpa maji safi ya kunywa, lilimhuzunisha, shirika hilo la habari lilisema.
Hata hivyo, iwapo anashikilia rekodi ya kukaa muda mrefu zaidi bila kuoga limekuwa suala la mjadala.
Mnamo 2009, kulikuwa na ripoti za mwanamume wa India ambaye – wakati huo – hakuosha au kupiga mswaki kwa miaka 35.
Kupiga mswaki na kuoga ni vitu viwili tofauti