RAIS Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi amewataka Watanzania kuvumiliana katika tofauti zao za kiimani. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).
Alhaj Mwinyi ametoa wito huo leo tarehe 31 Julai 2019, katika hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha Misingi 15 ya Amani, kilichoandikwa jijini Dar es Salaam na Mwanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Mohamed Iddi Mohamed.
Alhaj Mwinyi amewataka Watanzania kutodharau madhehebu ya dini “tuvumiliane katika dini zetu na madhehebu yetu, hapana shaka mtu anaamini madhehebu yake sawa sawa.
“Ndio ambayo akilala atapata usingizi, amhurumie mwingine, isiwe we mjinga hujui kitu ukitaka fuata hili langu, naye ataka usingizi vile vile,” amesema Alhaj Mwinyi na kuongeza:
“Basi tufanyeje, tuvumiliane katika madhehebu. Yako fuata vizuri namadhehebu ya mwenzio usiyadharau, dhahiri iheshimu, heshima ni mojawapo katika misingi ya dini.”
Kwenye uzinduzi huo Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amewakumbusha viongozi wa dini katika tasisi mbalimbali, Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na Watanzania kwa ujumla kuhamasisha wananchi kufuata misingi ya dini.
“Napenda niwakumbushe viongozi wa dini nchini hasa viongozi wa taasisi mbalimbali pamoja na wale BAKWATA viongozi wa mikoa, wilaya na maimamu wa misikiti.
“Umakini wa kiongoni una hitaji elimu uwezo na utayari. Sheikh akiwa kiongozi asiye na elimu ni vigumu kuwa makini,” amesema Sheikh Zubeir.
Leave a comment