Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Albino wakimbilia kwa Rais Magufuli
Habari Mchanganyiko

Albino wakimbilia kwa Rais Magufuli

Walemavu wa ngozi (Albino)
Spread the love

CHAMA cha wenye Ulemavu wa Ngozi Tanzania (TAS) kimemuomba Rais Dk. John Magufuli kutoa tamko la kukemea vikali vitendo vya ukatili kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) ili waweze kuishi kwa amani kama Watanzania wengine,” anaandika Christina Haule.

Mwenyekiti wa TAS , Nemes Temba amesema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari akikemea kitendo cha ukatili alichofanyiwa mwenzao, Nassoro Msingili (75) mkazi wa kijiji cha Nyarutanga kata ya Kisaki wilaya ya Morogoro vijijini Oktoba 3 mwaka huu.

Temba amesema kitendo cha Msingili kukatwa mkono kimewaumiza sana na anakemea vikali kwa kuwa tayari ameongeza ulemavu mwingine wa kukosa mkono wa kushoto.

Ametoa wito kwa viongozi wa dini, siasa na wadau wengine kutoa elimu kwa umma ili waweze kubadili mitazamo na kuacha kuwadhuru kutokana na kishirikina.

Aidha, aliliomba Jeshi la Polisi likiwa kusimamia usalama wa raia na mali zao kuwalinda watu kama linavyofanya kwa raia wengine.

Ameiomba serikali kufanya sensa ili kupata takwimu sahihi za walemavu wa ngozi kwa lengo la kutoa ulinzi imara dhidi yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!