Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko ALAT kuhamia mkoani Dodoma mwezi ujao
Habari Mchanganyiko

ALAT kuhamia mkoani Dodoma mwezi ujao

Mwenyekiti wa ALAT taifa, Gulamhafeez Mukadamu (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)
Spread the love

JUMUIYA ya Tawala ya Mitaa (ALAT) Tanzania inatarajia kuhamia mkoani  Dodoma ifikapo tarehe 1 mwaka huu, ikiwa ni  sehemu ya kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kuzitaka serikali kuhakia mkoani humo, anaandika Catherine Kayombo.

Mwenyekiti wa ALAT taifa, Gulam hafeez Mukadam, ametoa taarifa hiyo katika mkutano na wanahabari uliofanyika leo  idara ya habari na maelezo jijini Dar es salaam.

“Naunga mkono juhudi za rais kwa vitendo kwa kuhamishia shughuli za serikali makao makuu Dodoma, ambapo ALAT kuanzia tarehe mosi Agosti, 2017 ofisi za makao makuu zitahamia Dodoma”, alisema Mukadamu.

Katika mkutano huo, mwenyekiti  pia amekemea watumishi wa ALAT wasio waadilifu na kutoa taarifa ya hatua zitakazochukuliwa ili kuhakikisha kurejesha amani kwa wanajumuiya.

“Hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa watumishi wa sekretariat ya ALAT makao makuu ambao siyo waadilifu na wenye utendaji kazi usioridhisha”, aliongeza.

Mukadamu ametoa rai kwa mamlaka za serikali za mitaa kuendelea kuchangia chombo chao cha ALAT  kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi kwa manufaa ya wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!