Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko ALAT kuhamia mkoani Dodoma mwezi ujao
Habari Mchanganyiko

ALAT kuhamia mkoani Dodoma mwezi ujao

Mwenyekiti wa ALAT taifa, Gulamhafeez Mukadamu (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)
Spread the love

JUMUIYA ya Tawala ya Mitaa (ALAT) Tanzania inatarajia kuhamia mkoani  Dodoma ifikapo tarehe 1 mwaka huu, ikiwa ni  sehemu ya kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kuzitaka serikali kuhakia mkoani humo, anaandika Catherine Kayombo.

Mwenyekiti wa ALAT taifa, Gulam hafeez Mukadam, ametoa taarifa hiyo katika mkutano na wanahabari uliofanyika leo  idara ya habari na maelezo jijini Dar es salaam.

“Naunga mkono juhudi za rais kwa vitendo kwa kuhamishia shughuli za serikali makao makuu Dodoma, ambapo ALAT kuanzia tarehe mosi Agosti, 2017 ofisi za makao makuu zitahamia Dodoma”, alisema Mukadamu.

Katika mkutano huo, mwenyekiti  pia amekemea watumishi wa ALAT wasio waadilifu na kutoa taarifa ya hatua zitakazochukuliwa ili kuhakikisha kurejesha amani kwa wanajumuiya.

“Hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa watumishi wa sekretariat ya ALAT makao makuu ambao siyo waadilifu na wenye utendaji kazi usioridhisha”, aliongeza.

Mukadamu ametoa rai kwa mamlaka za serikali za mitaa kuendelea kuchangia chombo chao cha ALAT  kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi kwa manufaa ya wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!