Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Al-Shabab yatia doa uchaguzi Kenya
Makala & Uchambuzi

Al-Shabab yatia doa uchaguzi Kenya

Askari wa Al-Shabab
Spread the love

ZIKIWA zimebaki siku tano kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu nchini Kenya, hali ya usalama imeendelea kuwapa wasiwasi wananchi kufuatia mashambulizi pembezoni mwa pwani ya nchi hiyo, anaandika Catherine Kayombo.

Mashambulizi hayo yamefanyika maeneo ya Lamu, Mandera na maeneo ya jimbo la Lafey na wa watu wanaohisiwa kuwa Al-Shabab. Watu hao wamefanya mashambulizi ya mfululizo kwa siku mbili jumatano na Alhamis wakisababisha vifo vya watu takriban wanane.

Washambuliaji hao walivamia basi la abiria jana katika eneo la Lamu na kujeruhi watu watano. Pia Alhamis walivamia offisi za polisi katika Jimbo la Lafey na kuua polisi huku wengine wakijeruhiwa.

Kufuatia mashambulizi hayo, wakazi wa Pwani wamepata wasiwasi juu ya usalama wao kuelekea uchaguzi, kupelekea wengine kukimbia makazi yao. Wametoa rai kwa serikali kutozembea katika ulinzi hasa katika maeneo yanayoonekana kuwa hatarishi na yenye historia ya kuvamiwa na waasi.

Aidha, katibu katika wizara ya usalama joseph Bonieth amewahahakikishia wakazi wa Lamu na Mandera kuwa serikali itahakikisha ulinzi unakuwepo, na watu wasihame wala kukimbia maeneo yao kuhofia uvamizi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaMakala & Uchambuzi

Jeshi la Sudan lasitisha mazungumzo na wanamgambo wa RSF

Spread the love  JESHI rasmi la serikali ya Sudan, limesitisha ushiriki wake...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nimekomaa zaidi kisiasa katika miaka 9 ya ACT Wazalendo

Spread the love  LEO tarehe 5 Mei, ni ACT Dei. Ni siku...

Makala & Uchambuzi

Ulinzi hifadhi za Taifa uwe wa kila mtu

Spread the loveUJANGILI wa wanyamapori bado ni tatizo kubwa katika hifadhi za...

Makala & Uchambuzi

Miradi inayofadhiliwa na GGML inavyoleta mageuzi ya kiuchumi Geita

Spread the loveTANGU kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), ambayo ni...

error: Content is protected !!