WATU 18 wamepoteza maisha huku 15 wakijeruhiwa, katika ajali iliyohusisha lori la gari la abiria, iliyotokea asubuhi ya leo tarehe 15 Aprili 2020, mkoani Pwani. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Taarifa ya ajali hiyo imetolewa na Onesmo Lyanga, Kamanda Jeshi la Polisi mkoa wa kipolisi wa Rufiji.
Kamanda Lyanga amesema ajali hiyo imetokea kwenye kijiji cha Kilimahewa wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani, baada ya gari hilo kugongana na lori.
Amesema majeruhi wanapatiwa matibabu katika Kituo cha Afya cha Kilimahewa.
Amesema gari la abiria lilikuwa linatokea mikoa ya Kusini kwenda jijini Dar es Salaam.
Leave a comment