Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ajali ya Ndege Serengeti: Wawili wafariki
Habari Mchanganyiko

Ajali ya Ndege Serengeti: Wawili wafariki

Ajali ya Ndege
Spread the love

WATU wawili wamefariki dunia katika ajali ya ndege iliyotokea asubuhi ya leo tarehe 23 Septemba 2019, kwenye uwanja wa ndege mdogo wa Seronera uliko kwenye hifadhi ya Serengeti mkoani Mara. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa ya ajali hiyo imetolewa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Taarifa ya TANAPA inaeleza kuwa, ajali hiyo imetokea baada ya ndege ndogo ya Kampuni ya Auric Air kuanguka katika uwanja wa Seronera.

“Ndege ya Kampuni ya Auric Air imeanguka leo asubuhi katika uwanja mdogo wa ndege Seronera, Serengeti. Rubani mmoja na abiria mmoja wamepoteza maisha. Taarifa zaidi zitatolewa.Rubani na abiria wote ni raia wa Tanzania,” inaeleza taarifa ya TANAPA.

Pascal Shelutete, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Mawasiliano TANAPA amesema ndege hiyo ilikuwa na watu wawili ambao wote wamefariki dunia.

Shelutete amesema, mamlaka husika zitatoa taarifa zaidi juu ya chanzo cha ajali hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!