Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Ajali ya Ndege Serengeti: Wawili wafariki
Habari Mchanganyiko

Ajali ya Ndege Serengeti: Wawili wafariki

Ajali ya Ndege
Spread the love

WATU wawili wamefariki dunia katika ajali ya ndege iliyotokea asubuhi ya leo tarehe 23 Septemba 2019, kwenye uwanja wa ndege mdogo wa Seronera uliko kwenye hifadhi ya Serengeti mkoani Mara. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa ya ajali hiyo imetolewa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Taarifa ya TANAPA inaeleza kuwa, ajali hiyo imetokea baada ya ndege ndogo ya Kampuni ya Auric Air kuanguka katika uwanja wa Seronera.

“Ndege ya Kampuni ya Auric Air imeanguka leo asubuhi katika uwanja mdogo wa ndege Seronera, Serengeti. Rubani mmoja na abiria mmoja wamepoteza maisha. Taarifa zaidi zitatolewa.Rubani na abiria wote ni raia wa Tanzania,” inaeleza taarifa ya TANAPA.

Pascal Shelutete, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Mawasiliano TANAPA amesema ndege hiyo ilikuwa na watu wawili ambao wote wamefariki dunia.

Shelutete amesema, mamlaka husika zitatoa taarifa zaidi juu ya chanzo cha ajali hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!