Monday , 29 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Ajali mbaya yatokea Songwe, yaua abiria wote
Habari Mchanganyiko

Ajali mbaya yatokea Songwe, yaua abiria wote

Spread the love

WATU 19 wamepoteza maisha kutokana na ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika eneo la Senjele mkoani Songwe. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akithibitisha kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Songwe, SACP, George Simba Kiando amesema ajali hiyo iliyohusisha lori lenye namba za usajili T825 CMJ na gari la abiria aina ya Coaster (T269 CJC), ilitokea majira ya saa tatu na robo usiku.

Kamanda Kiando amesema chanzo cha ajali hiyo ni breki ya Lori kushindwa kufanya kazi katika mteremko wa mpakani mwa mkoa wa Mbeya na Songwe na kulikopelekea roli hilo kuigonga Coaster iliyokuwa na abiria 18 na kusababisha vifo hivyo.

Ameeleza kuwa, watu 17 akiwemo dereva wa roli walifariki papo hapo wakati wawili walifariki dunia wakati wakipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Kamanda Kiando amesema katika vifo hivyo, watu 14 walikuwa wanawake na 5 walikuwa wanaume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

Habari Mchanganyiko

Kampeni ya Samia Legal Aid yazinduliwa Manyara, kesi 45 zapokelewa

Spread the love  KAMPENI ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia, imezinduliwa...

Habari Mchanganyiko

NMB ya kwanza kuzindua Malipo kwa QR na UnionPay International

Spread the loveBENKI ya NMB kwa kushirikiana na UnionPay International (UPI), wamezindua...

error: Content is protected !!