Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ajali mbaya yatokea Songwe, yaua abiria wote
Habari Mchanganyiko

Ajali mbaya yatokea Songwe, yaua abiria wote

Spread the love

WATU 19 wamepoteza maisha kutokana na ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika eneo la Senjele mkoani Songwe. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akithibitisha kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Songwe, SACP, George Simba Kiando amesema ajali hiyo iliyohusisha lori lenye namba za usajili T825 CMJ na gari la abiria aina ya Coaster (T269 CJC), ilitokea majira ya saa tatu na robo usiku.

Kamanda Kiando amesema chanzo cha ajali hiyo ni breki ya Lori kushindwa kufanya kazi katika mteremko wa mpakani mwa mkoa wa Mbeya na Songwe na kulikopelekea roli hilo kuigonga Coaster iliyokuwa na abiria 18 na kusababisha vifo hivyo.

Ameeleza kuwa, watu 17 akiwemo dereva wa roli walifariki papo hapo wakati wawili walifariki dunia wakati wakipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Kamanda Kiando amesema katika vifo hivyo, watu 14 walikuwa wanawake na 5 walikuwa wanaume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!