Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Aibu mtuhumiwa kufia mikononi mwa polisi- Rais Samia
Habari za Siasa

Aibu mtuhumiwa kufia mikononi mwa polisi- Rais Samia

IGP Simon Sirro
Spread the love

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Polisi kuacha kutumia nguvu kubwa katika utekelezaji wa majukumu yake ili kuondoka na aibu ya watuhumiwa kufia mikononi mwao. Anaripoti Gabriel Mushi, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa agizo hilo leo Jumatano tarehe 25 Agosti, 2021 wakati akifungua kikao kazi cha maofisa wakuu waandamizi wa jeshi la polisi na makamanda wa polisi wa mikoa/vikosi – Oysterbay Dar es salaam.

“Kumekuwapo na matumizi makubwa ya nguvu. Hili nalo naomba mlitizame…kesi za watu kufariki kwenye vituo vya polisi haipendezi machoni kwa watu, tendeni yaliyo haki,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema kuna watuhumiwa wengine ni ngangari hata kama askari akimchapa virungu vya kutosha lakini kuna wengine virungu viwili tu amepoteza maisha.

Amesema baadhi ya askari wanashutumiwa kutofanya haki kwa jamii na inapotokea wakakiuka maadili ya kazi wanasimama haraka kujitetea kama jeshi bila kuangalia haki za jamii.

“Kwa mfano miezi miwili mitatu nyuma kulikuwa na unyang’anyi wa nyama kwenye mabucha hapa Dar, Polisi mlipolalamika mkasema tumefanya vile kwa sheria, lakini ukiangalia kilichotendeka hakuna sheria hapa, muangalie na hili, mpo hapa kuhudumia watu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!