Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Ahmed Ally afunguka ubora wa Fiston Mayele
HabariMichezo

Ahmed Ally afunguka ubora wa Fiston Mayele

Spread the love

 

MARA baada ya kuibuka mjadala kwenye mitandao ya kijamii juu ya ubora wa mshambuliaji wa klabu Yanga Fiston Mayele, Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba Ahmed Ally amesema kuwa mchezaji huyo anakitu ndani yake kinachomfanya kuwa bora na kujitofautisha na wengine. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Ahmed aliyasema hayo kwenye moja ya kipindi cha uchambuzi wa Magezeti, hii leo tarehe 12 Aprili 2022, wakati wakipitia kurasa mbalimbali za michezo kwenye magazeti hayo.

Katika mjadala huo Ahmed alisema kuwa, mpira wa miguu ni mchezo wa namba, na mpaka sasa mshambuliaji huyo ameshapachika jumla ya mabao 11 na kwenye Ligi Kuu kunawashambuliaji ambao wamecheza mismu mitano na hawajafikisha idadi hiyo ya mabao.

“Mpira ni mchezao wa namba anamagoli 11 ndio kinara ukisema sio bora inabidi ututajie bora.”

“Kuna washambuliaji wengi wanacheza hii Ligi kwa msimu mitano au minne, hawajawahi kufikisha mabao 10 kwa hiyo ana kitu unaweza kumpongeza kwa kile kitu ambacho anacho.” Alisema Ahmed

Mjadala juu ya ubora wa mshambuliaji huyo uliibuliwa hivi karibuni na msemaji wa klabu ya Azam FC, Thabiti Zakaria maarufu kama Zaka za Kazi, mara baada ya kunukuliwa akisema kuwa mchezaji huyo ni wakawaida sana tofauti na watu wanavyomsifia.

Mpaka sasa kwenye Ligi Kuu Tanzania mara baada ya kupigwa kwa michezo 19, mshambuliaji huyo raia wa kidemokrasia ya Congo, ameshapachika jumla ya mabao 11na kumfanya kuwa kinara kwenye msimamo wa wafungaji.

Aidha Meneja huyo aliendelea kusema kuwa, kwa upande wake Mayele ni mchezaji mzuri kwa kuwa anakitu ndani yake na kufunga mabao 10 sio jambo dogo.

“Kwangu mimi ni mchezaji mzuri kufunga mabao 10, kwenye Ligi aliyocheza kwa mara ya kwanza si jambo dogo, anakitu ndani yake ambacho anacho.” Alisema Meneja habari huyo

Mshambuliaji huyo alisajiliwa na Yanga kwenye diorisha kubwa la usajili kwa mkataba wa miaka miwili, akitokea kwenye klabu ya AS Vita inayoshiriki ligi Kuu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huku ukiwa ni msimu wake wa kwanza kukipiga ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!