Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ahadi ya Kikwete abebeshwa Rais Magufuli
Habari za Siasa

Ahadi ya Kikwete abebeshwa Rais Magufuli

Rais John Magufuli akiwa na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete
Spread the love

 

MBUNGE wa Same Magharibi, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), David Mathayo David, amehoji ni lini Serikali ya awamu ya tano inayongozwa na Rais John Magufuli, itaanza kutekeleza mradi wa ujenzi wa daraja la Mto Pangani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni katika kipindi cha maswali na majibu leo Jumatano tarehe 10 Februari 2021, David amesema ujenzi wa daraja hilo ilikuwa ahadi ya Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete.

David amesema, ahadi hiyo ya Kikwete, aliyekuwa Rais kati ya mwaka 2005-2015, ililenga kuondoa adha ya usafiri kwa wakazi wa jimbo lake.

“Safari ya Kutoka Kilimanjaro kwenda Dodoma kupitia Same na Simanjiro, huweza kufupishwa kwa zaidi ya kilomita 180 na kupunguza usumbufu.

“Je, ile ahadi ya Rais wa awamu ya nne (Rais Kikwete) ya kujenga Daraja la Mto Pangani mpakani mwa Wilaya ya Same na Simanjiro, utaanza lini?” amehoji David.

Rais Kikwete alimaliza muda wake wa uongozi wa vipindi viwili mfululizo (2005-2015), Novemba 2015, kisha alikabidhi kijiti kwa Rais Magufuli.

Ikijibu swali, Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais-Tamisemi imesema, serikali imepanga kutenga kiasi cha fedha katika bajeti ya mwaka 2021/2022, kwa ajili ya kufanya usanifu wa daraja hilo, kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini (Tarura).

Wizara hiyo imeeleza, usanifu huo utafanyika katika eneo ambalo kutajengwa daraja pamoja na barabara itakayounganisha Wilaya za Same na Simanjiro.

David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi (CCM)

“Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22, Tarura imepanga kufanya usanifu wa daraja ikiwa ni pamoja na kipande cha barabara yenye urefu wa kilomita 34.2 kwa upande wa Same hadi kufikia eneo la Mto Pangani. Panapohitajika kujengwa daraja ili kuunganisha Wilaya za Same na Simanjiro,” imeeleza wizara.

Aidha, wizara hiyo imeeleza, Tarura imekuwa ikihudumia kipande cha barabara hiyo kwa kufanya matengenezo kwenye maeneo korofi, ambapo kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019 Sh. 48 Mil zilitumika kwa ajili ya shughuli hiyo.

“Aidha, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2020/21 kiasi cha Sh.63 milioni, kimetengwa kwa ajili ya matengenezo ambapo kwa sasa mkandarasi anaendelea na matengenezo ya kipande cha kilomita 7,” imelezwa.

Na kwamba, serikali itatoa kipaumbele cha ujenzi wa daraja na miundombinu ya barabara muhimu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!