Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ahadi ya Dk. Bashiru kwa wagombea CCM
Habari za Siasa

Ahadi ya Dk. Bashiru kwa wagombea CCM

Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM
Spread the love

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally, ameahidi kuwapitisha kwenye ‘tanuri’ wagombea wa chama hicho kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa utaofanyika tarehe 24 Novemba 2019. Anaandika Regina Mkonde…(endelea).

Akihojiwa na gazeti moja la kila siku, Dk. Bashiru amesema, mwanachama yeyote wa chama hicho anayetaka kugombea nafasi ya uenyekiti wa mtaa au wa kijiji, atajadiliwa na kamati ya siasa ya tawi.

Na kwamba katika mchakato wa kuteua wagombea, hakutakuwa na mianya ya rushwa wala upendeleo, bali utafanyika kwa uwazi kwa kuzingatia misingi ya demokrasia.

“Kabla ya kupigiwa kura za maoni, atajadiliwa kwanza na kamati ya siasa ya tawi lake na kamati ya siasa ya kata na hatimaye kamati ya siasa ya wilaya itafikiria na kuteua majina ya WanaCCM wasiozidi watatu kwa kila kijiji.

“… ama mtaa walioomba kugombea uenyekiti wa kijiji ama mtaa ili wakapigiwe kura za maoni na mkutano wa wanachama wote katika tawi husika,” amesema Dk. Bashiru.

Dk. Bashiru amesema baada ya wahusika kujadiliwa na kamati ya siasa ya tawi au kata, wanachama wa eneo husika watawapigia kura za maoni kwa ajili ya kumpata MwanaCCM atakayepeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!