Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Agizo la Rais Samia: Mwigulu aibana TRA
Habari za Siasa

Agizo la Rais Samia: Mwigulu aibana TRA

Spread the love

 

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba ameiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kufuata sheria na taratibu za nchi katika ukusanyaji mapato, pasi na kuwaathiri walipakodi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Dk. Mwigulu ametoa agizo hilo leo Jumamosi tarehe 3 Aprili 2021 jijini Dodoma, akizungumza na watendaji wa taasisi na idara zilizoko katika Wizara ya Fedha na Mipango.

“Sheria zipo, taratibu zipo na zoezi hili linafanywa na wataalamu ambao wabobezi.  Turekebishe pale ambapo tumeenda kinyume na sheria na weledi wetu, turudi kweye mstari ili tulinde uchumi wetu vilevile tusiuwe walipa kodi,” ameagiza Dk. Mwigulu.

Agizo hilo ni utekelezwaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan alilolitoa hivi karibuni kwa wizara hiyo, akiitaka isiwabebeshe mzigo mkubwa walipa kodi, ili kuzuia baishara kufungwa kutokana na wafanyabaishara kushindwa kulipa kodi hizo.

“Ili tuweze kuendelea kupata mapato makubwa katika nchi yetu ni lazima tukuze uchumi, lazima uchumi uwepo ndiyo tunaweza kupata mapato, rais hili aliliangalia na kulipa uzito mkubwa kwamba lazima tulinde uchumi wetu, maana yake tukuze uchumi wetu tutapata wigo mpana kukusanya kodi,” amesema Dk. Mwigulu.

Waziri huyo wa fedha amesema  “Sisi wizara pamoja na taasisi lazima tulifanyie kazi na tutekeleze ipasavyo, kwa hiyo kila mtu kwa idara yake ajipange nalo na liwe kiapumbele, tukuze uchumi tuzalishe walipa kodi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!