Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Afya ya Mbowe yazidi kuimarika
Habari za Siasa

Afya ya Mbowe yazidi kuimarika

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

AFYA ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe inazidi kuimalika baada ya kufikishwa kwenye hospitali na Rufaa ya KCMC jana jioni akiwa huku afya yake ikiwa sio shwari. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa Msemaji wa hospitali hiyo, Gabriel Chisseo ameeeza kuwa Kiongozi huyo wa kambi ya upinzani bungeni alifikishwa hospitali hapo akiwa na maumivu makali ya kichwa. 

Chisseo ameeleza kuwa baada ya kufanyiwa uchunguzi wa awali zinaonesha mbunge huyo ana uchovu.

“Taarifa zinaonyesha alikuwa na maumivu ya kichwa. Taarifa za kitabibu zinaonyesha ni uchovu,” ameeleza Chisseo.

Chasseo ameleeza kuwa Mbowe amepumzishwa kwenye hosiptali hiyo akiendelea kupatiwa matibabu na kwamba anaendelea vizuri. “Wataalamu wanaendelea kumhudumia kwa ukaribu baadaye atafanyiwa vipimo vingine.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!