Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yawatwisha vijana zigo la ugumu wa maisha
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yawatwisha vijana zigo la ugumu wa maisha

Spread the love

 

VIJANA wametakiwa kushirikiana katika kuleta uhuru wa kiuchumi, ili kuondoa changamoto ya ugumu wa maisha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo imetolewa hivi karibuni na Naibu Msemaji wa Vijana, Kazi na Ajira, wa Chama cha ACT-Wazalendo, Felix Kamugisha, katika ziara yake aliyofanya kwenye maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Kamugisha alisema vijana wa zamani wakiongozwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, walipambana kuleta uhuru wa kujitawala, hivyo vijana wa Sasa wanapaswa kupigania uhuru wa uchumi na kuchagua viongozi wanaowataka wawaongoze kwa kulinda maslahi Yao.

“Sisi vijana tunatakiwa kufanya mabadiliko ya nchi yetu, waliopigania uhuru walikuwa vijana mpaka leo tuko huru lakini hatuko huru kiuchumi, kuchagua wawakilishi Wetu bungeni,” alisema Kamugisha.

Kamugisha alisema “matatizo hata tuliyokuwa nayo sio bahati mbaya, wala hayakutoka kwa Mungu, yanasababishwa na watu tuliowapa dhamana ya kutuongoza. Badala ya kulinda maslahi yetu lakini wanakwenda bungeni kupanga ambayo hatujawatuma sisi.”

Msemaji huyo wa Vijana ACT-Wazalendo, alisema kundi hilo linapaswa kuhakikisha linajitokeza kushiriki katika chaguzi mbalimbali, ili kuchagua viongozi wazalendo watakaotumia rasilimali za nchi kuleta maendeleo na kutatua changamoto zao, ikiwemo ukosefu wa Ajira.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!