Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yawaonya wanaotaka kukiendesha, kukiburuza
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yawaonya wanaotaka kukiendesha, kukiburuza

Ado Shaibu, Katibu Mkuu ACT-Wazalendo
Spread the love

 

KATIBU Mkuu wa Chama cha ACT- Wazalendo nchini Tanzania, Ado Shaibu, amesema chama chake kinataka kujitofautisha na vyama vingine, hivyo hakitakubali kuendeshwa kwa kuburuzwa na au msukumo kutoka kwa chama kingine. Anaripoti Mwandishi Wetu, Ruvuma … (endelea).

Ado ametoa kauli hiyo jana Jumanne, tarehe 21 Desemba 2021, akielezea hostia ya kuanzishwa kwa ACT-Wazalendo mwaka 2014, wakati akizungumza na wanachama wake wa Wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma.

“Lazima mfahamu chama hiki hakitoendeshwa kwa matakwa ya chama kingine chochote cha siasa, ACT-Wazalendo hakitoendeshwa wala kuburuzwa na maelekezo, msukumo na ushawishi wa chama kingine chochote cha siasa. Kitaendeshwa kwa misngi ambayo tumejiwekea kwenye katiba,” amesema Ado.

Katibu Mkuu huyo wa ACT-Wazalendo, amesema chama hicho kinataka kujitofautisha na vyama vingine kwa kuwa mfano kwenye siasa za kistaarabu na za kuwakomboa Watanzania masikini kiuchumi.

“Kwa hiyo chama hiki kinataka kujitofautisha na vyama vingine, tunataka kuwa chama bora na cha mfano ambacho kitajipambanua kwa siasa za kistaarabu, za kuwakomboa Watanzania masikini na siasa za masuala ya maslahi ya wakulima, wafanyakazi na wafanyabiashara,” amesema Ado.

Ado amesema, ACT-Wazalendo kilianzishwa baada ya kuona Tanzania inakosa siasa zisizojikita katika kutatua matatizo ya wananchi.

Ado Shaibu, Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo akizungumza na wanachana wa chama hicho katika jimbo la Nyasa mkoani Ruvuma.

“Wakati chama hiki kinaanzishwa mwaka 2014, ni muhimu mfahamu kilizaliwa kutokana na mapungufu. Nchi nzima lazima wafahamu hili, kulikuwa na upungufu wa mfumo wa uendeshaji siasa za nchi yetu, siasa ziligubikwa na ubabaishaji, kukosa uwazi, uadilifu na kukosekana kwa uzalendo,” amesema Ado na kuongeza:

“Siasa ziligubikwa na viongozi ambao wanamsahau mwananchi mnyonge wa vijijini na mjini, viongozi wa vyama tulikuwa hatujajikita katika siasa za kumkomboa mwananchi masikini. Ndiyo zilikuwa siasa za Tanzania.”

Ado yuko katika ziara ya Sekretarieti ya ACT-Wazalendo Taifa, iliyoanza tarehe 20 Desemba mwaka huu, ambapo atatembelea mikoa ya Ruvuma, Mtwara, Lindi, Pwani na Tanga.

Ziara hiyo inalenga kukijenga chama hicho ikiwa pamoja na kuwaandaa wanachama wake kuhusu mabadiliko ya uendeshaji wake kisayansi .

Kauli hiyo ya Ado imekuja siku kadhaa baada ya baadhi ya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kukosoa hatua ya Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ya kumuombea radhi mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, anayesota rumande miezi mitano, akikabiliwa na mashtaka ya ugaidi.

Zitto alitumia kikao cha wadau wa tasnia ya siasa, kilichoandaliwa na Baraza la Vyama vya Siasa nchini, ambacho Chadema kiligoma kushiriki, kumuomba Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amsamehe Mbowe ili aachwe huru kwa ajili ya kujenga umoja wa kitaifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!