Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yawaita viongozi wa dini, wastaafu kutuliza joto
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo yawaita viongozi wa dini, wastaafu kutuliza joto

Mbarara Maharagande, Katibu wa Idara ya Haki za Binadamu na Makundi Maalumu ya Chama cha ACT-Wazalendo
Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimewataka viongozi wa dini na viongozi wa serikali waliostaafu kukemea hujuma zinazojitokea katika uchaguzi Serikali za Mitaa kwani zinaweza kusababisha uvunjifu wa amani. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mbarala Maharagande, Mratibu wa Mawasiliano wa Uchaguzi wa Serikali Mitaa ndani ya ACT-Wazalendo, amesema viongozi wa dini na wale wastaamu wamekuwa mstari wa mbele kuhimiza amani nchini lakini wamekuwa kimya kukemea vitendo vinavyoashiria kupotea kwa amani wanayoinadi kila siku.

 “Viongozi wa dini na wastaafu mara nyingi wamekuwa wakisisitiza na kuhamasisha kulinda amani, lakini hawaonekani kuhimiza kutendwa kwa haki na kukemea viashiria vya kupotea kwa amani na utulivu,” amesema Maharagande.

Amedai kuwa endapo vitendo vinavyofanywa na wasimamizi wa uchaguzi visipokemewa vitaharibu uchaguzi.

Amesema kuwa kinachodaiwa kuwa ni dosari na Waziri wa Tamisemi, Suleman Jaffo siyo kweli, ukweli ni hujuma zinafanyika kwa vyama vya upinzani.

Amezitaja miongoni mwa hujuma wanazozidai ni Serikali kutofanya maandalizi yanayostahili juu ya uchaguzi huu na kufungwa ofisi za wasimamizi wa uchaguzi, kukosekana mihuri, vitisho na, wasimamizi kudai mambo yasiyoelezwa na kanuni na sheria (utambulisho toka Mkoani), jeshi la polisi kutochukua hatua sahihi kudhibiti uhalifu.

Amezitaka mamlaka zinazohusika kudhibiti matendo yanayofanywa na watendaji hao yatakayosababisha kupandikiza chuki, uhasama miongoni mwa jamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!