Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yatoa neno wanaokihama chama
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo yatoa neno wanaokihama chama

Spread the love

KATIBU wa Itikadi na mawasiliano ya umma wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu amesema wimbi la wanachama wa chama hicho kuhamia CCM linakikomaza, anaandika Hamis Mguta.

Shaibu amesema hayo leo asubuhi katika mahojiano yake na kituo kimoja cha redio hapa nchini wakati  akizungumzia hali ya chama baada ya wimbi la wanachama wao kuendelea kuwakimbia.

“Siasa zinahitaji watu na viongozi makini, lakini tulishachora mstari baada ya kamati ya uongozi kukaa, Mwigamba na baadhi ya viongozi wana maoni ya kwamba tunakokwenda siyo sahihi na sisi wenyewe tunaamini kwamba tupo sahihi, ACT sasa ni chama cha kiaharakati,” amesema.

Amesema kuwa kama yupo mtu haridhiki juu ya msimamo wao  wa kupambana na serikali atoke. “Mtu akiondoka kwa sababu unapambana zaidi na serikali anakusaidia sana”

Amesema kuwa wanaowaza kuwa Zitto Kabwe yupo mbioni kuondoka katika chama hicho ni maono yao, lakini kama msemaji wa chama hana taarifa za Zitto kutaka kuondoka katika chama hiko na kurudi Chadema.

“Sijawahi kusikia mpango huo na sijawahi kuona kwa sababu mimi ndiyo msemaji wa chama na nashirikiu kuwepo kwenye vikao vyote na nafanya mawasiliano na viongozi wote,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!