KATIBU wa Itikadi na mawasiliano ya umma wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu amesema wimbi la wanachama wa chama hicho kuhamia CCM linakikomaza, anaandika Hamis Mguta.
Shaibu amesema hayo leo asubuhi katika mahojiano yake na kituo kimoja cha redio hapa nchini wakati akizungumzia hali ya chama baada ya wimbi la wanachama wao kuendelea kuwakimbia.
“Siasa zinahitaji watu na viongozi makini, lakini tulishachora mstari baada ya kamati ya uongozi kukaa, Mwigamba na baadhi ya viongozi wana maoni ya kwamba tunakokwenda siyo sahihi na sisi wenyewe tunaamini kwamba tupo sahihi, ACT sasa ni chama cha kiaharakati,” amesema.
Amesema kuwa kama yupo mtu haridhiki juu ya msimamo wao wa kupambana na serikali atoke. “Mtu akiondoka kwa sababu unapambana zaidi na serikali anakusaidia sana”
Amesema kuwa wanaowaza kuwa Zitto Kabwe yupo mbioni kuondoka katika chama hicho ni maono yao, lakini kama msemaji wa chama hana taarifa za Zitto kutaka kuondoka katika chama hiko na kurudi Chadema.
“Sijawahi kusikia mpango huo na sijawahi kuona kwa sababu mimi ndiyo msemaji wa chama na nashirikiu kuwepo kwenye vikao vyote na nafanya mawasiliano na viongozi wote,” amesema.
Leave a comment