Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yapaza sauti uhuru wa Sahara Magharibi
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yapaza sauti uhuru wa Sahara Magharibi

Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimeishauri Serikali ya Morocco iitishe kura ya maoni ili wananchi wa Sahara Magharibi, waamue kama wanakubali kuwa Taifa huru au waendelee kutawaliwa na serikali hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wito huo umetolewa leo Jumanne, tarehe 17 Mei 2022 na Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, akizungumza katika maadhimisho ya miaka 100 ya kuzaliwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Ado amesema, endapo Serikali ya Morocco itaacha kuitawala nchi ya Sahara Magharibi, kinyume na sheria za kimataifa na haki ya nchi kujitawala na kujiamulia mambo yake, wataenzi msimamo wa Mwalimu Nyerere wa kupinga nchi za Afrika kuendelea kutawaliwa.

“Ninafurahi kuyasema haya mbele ya Balozi wa Sahara Magharibi Ndugu Mahyub Sidina na Maafisa Waandamizi wa Ubalozi wa Morocco ambao mmehudhuria maadhimisho haya. Tanzania, kwa mujibu wa Mwalimu Nyerere, haiwezi kusemwa kuwa huru kama kuna Nchi yoyote ndani ya Afrika inaendelea kutawaliwa”-amesema Ado na kuongeza:

“Kitendo cha Morroco kuendelea kuikalia Sahara Magharibi kimabavu tangu 1975 hakikubaliki. Tunatoa wito wa kufanyika kura ya maoni ya Wananchi wa Sahara Magharibi, kuamua hatma yao kama ilivyoazimiwa na Umoja wa Mataifa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kura ya Maoni ya Sahara Magharibi (MINURSO), ukaundwa 1991.”

Maadhimisho ya Miaka 100 ya Kuzaliwa kwa Mwalimu Nyerere yalihudhuriwa na Viongozi Mbalimbali wa Serikali, Mabalozi, Wanazuoni, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Vyama vya Kisiasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!