Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yamtaka CAG afanye ukaguzi maalum fedha za muungano
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yamtaka CAG afanye ukaguzi maalum fedha za muungano

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Charles Kichere
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimeitaka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), afanye ukaguzi maalum kwenye mapato na matumizi ya fedha za muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ili kubaini kama zinagawiwa inavyostahili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ushauri huo umetolewa leo Alhamisi, tarehe 16 Juni 2022, jijini Dar es Salaam na Msemaji wa Kisekta wa Fedha wa ACT-Wazalendo, Emmanuel Mvula, akichambua makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2022/23.

“Tunamshauri CAG afanye ukaguzi maalum wa fedha za muungano, mapato, matumizi na fedha zinazobaki ili kubainisha mgawo sahihi fedha ambazo Zanzibar inastahili,” amesema Mvula.

Katika hatua nyingine, Mvula amesema chama chake kinashauri Serikali ifanye upya utafiti wa mapato ya muungano huo, ili kupata takwimu sahihi.

Aidha, Mvula amesema chama chake kinashauri Serikali ianzishe akaunti ya pamoja ya fedha kwa mujibu wa sheria na mapato yote ya muungano yawekwe katika akaunti hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!