MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, amesema amebaini upotevu wa kodi ya zuio ya Sh 749 uliotokana na kutokukusanywa na kuwasilishwa katika Mamlaka ya Mapato Tanzania. Anaripoti Eliabu Kanyika, DSJ … (endelea).
Miongozi mwa taasisi sita zilizotajwa kukusanya kodi hiyo na kutoiwasilisha TRA ni Chama cha ACT-Wazalendo ambacho kilizuia Sh 8.5 milioni lakini haikuwasilisha TRA.
Kicheere amebainisha hayo leo Jumatano tarehe 29 Machi 2023 Ikulu ya Dar es salam akimkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan Ripoti ya Taarifa za Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2021/2022.
Amesema taasisi 6 zilizuia kodi lakini hazikuwasilisha TRA Sh milioni 35 kinyume cha sheria.
Alisema taasisi 15 hazikukata kodi ya zuio ya Tsh 713.70 Milioni na taasisi 6 zilizuia kodi na hazikuwasilisha TRA Sh 35 milioni.
Mbali na ACT-Wazalendo taasisi zingine Wizara ya Viwanda na Biashara Sh. 16 milioni.
Taasisi ambazo hazikukusanya kodi ya zuio ni Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Sh 442 milioni, Kampuni ya Ujenzi ya JKT Sh 162 milioni, Wakala wa Usambazaji Maji Vijijini (RUWASA) Sh. 56 milioni na Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (TANEPS) Sh 34 Milioni.
Mbali na hilo Kicheere ameeleza kuwa wamebaini ukusanyaji wa mapato nje ya mfumo wa GePG ambapo RUWASA ilikusanya Sh 68 bilioni, Tume ya Teknolojia ya Habari na Mawasilino Sh 151 bilioni na Shirika la Magereza Sh 900.96 milioni.
“Zote zimekusanywa nje ya GePG na ni kukiuka maelekezo ya Serikali inayoelekeza fedha zote zikusanywe kwa mfumo huo,” amesema Kicheere.
Pia upotevu mwingine wa mapato ni kutokukusanywa kwa ada ya usafirishaji wa mizigo iliyozidi uzito iliyoidhinishwa na Wizara ya Ujenzi na kupoteza mapato ya Sh 41.48 bilioni.
Aidha TBA kutokukusanya kwa kodi za nyumba zilizopangishwa kwa taasisi za Serikali kwa muda wa miezi 10 na kuendelea na hivyo kupoteza mapato ya Sh 13 bilioni.
Leave a comment