Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo: Ni uchungu kumpoteza Maalim Seif
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo: Ni uchungu kumpoteza Maalim Seif

Bendera ya ACT-Wazalendo
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo nchini Tanzania kimesema, kimeshtushwa na kifo cha mwenyekiti wake, Maalim Seif Sharif Hamad, kilichotokea leo Jumatano tarehe 17 Februari 2021, kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema, chama hicho kimepata pigo kubwa kwa kuondokewa na kiongozi wake.

Zitto amesema, hakuna maneno ambayo anaweza kuyaelezea kuhusu kifo cha Maalim Seif (77), kwa kuwa Mungu mwenyewe amemua kumchukua mja wake.

“Hakuna maneo ambayo, tunaweza kuyaeleza kwa wanachama, Wazanzibar na kwa Watanzania kwa ujumla kuhusiana na uchungu mkubwa wa taarifa hii, lakini sisi sote ni wa Mungu na kwake tutarejea,” amesema Zitto kwa uchungu mkubwa.

Akizungumza kwa upole, Zitto amesema, alikwenda Muhimbili asubuhi ya leo kwa ajili ya kumjulia hali Maalim Seif, na kwamba alielezwa na jopo la madaktari waliokuwa wanamuangalia mwanasiasa huyo, kwamba hali yake kiafya inaonyesha matumaini.

“Kwa mujibu wa taarifa ya madaktari na leo asubuhi nilikuwa hospitalini mpaka saa 2.00 asubuhi, nilikuwa hospitalini Muhimbili na kuzungumza na jopo la madaktari waliokuwa wanamhudumia na hali yake ilikuwa inatia matumaini.”

Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe katikati akiwa na katibu mkuu wa chama hiko Ado Shaibu (kushoto) pamoja na Makamu Mwenyekiti wake Doroth Temu (kulia)

“Hata hivyo, mnano saa 5:26 asubuhi, mwenyezi Mungu alitwaa roho yake,” amesema Zitto

Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo amesema, taratibu za mazishi zitatolewa baada ya kuwasiliana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!