Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo: Ni uchungu kumpoteza Maalim Seif
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo: Ni uchungu kumpoteza Maalim Seif

Bendera ya ACT-Wazalendo
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo nchini Tanzania kimesema, kimeshtushwa na kifo cha mwenyekiti wake, Maalim Seif Sharif Hamad, kilichotokea leo Jumatano tarehe 17 Februari 2021, kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema, chama hicho kimepata pigo kubwa kwa kuondokewa na kiongozi wake.

Zitto amesema, hakuna maneno ambayo anaweza kuyaelezea kuhusu kifo cha Maalim Seif (77), kwa kuwa Mungu mwenyewe amemua kumchukua mja wake.

“Hakuna maneo ambayo, tunaweza kuyaeleza kwa wanachama, Wazanzibar na kwa Watanzania kwa ujumla kuhusiana na uchungu mkubwa wa taarifa hii, lakini sisi sote ni wa Mungu na kwake tutarejea,” amesema Zitto kwa uchungu mkubwa.

Akizungumza kwa upole, Zitto amesema, alikwenda Muhimbili asubuhi ya leo kwa ajili ya kumjulia hali Maalim Seif, na kwamba alielezwa na jopo la madaktari waliokuwa wanamuangalia mwanasiasa huyo, kwamba hali yake kiafya inaonyesha matumaini.

“Kwa mujibu wa taarifa ya madaktari na leo asubuhi nilikuwa hospitalini mpaka saa 2.00 asubuhi, nilikuwa hospitalini Muhimbili na kuzungumza na jopo la madaktari waliokuwa wanamhudumia na hali yake ilikuwa inatia matumaini.”

Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe katikati akiwa na katibu mkuu wa chama hiko Ado Shaibu (kushoto) pamoja na Makamu Mwenyekiti wake Doroth Temu (kulia)

“Hata hivyo, mnano saa 5:26 asubuhi, mwenyezi Mungu alitwaa roho yake,” amesema Zitto

Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo amesema, taratibu za mazishi zitatolewa baada ya kuwasiliana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!