Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo: Mghwira ameacha historia
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo: Mghwira ameacha historia

Anna Mghwira, Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimemlilia aliyekuwa mwenyekiti wake wa kwanza, Anna Mghwira, kikisema kwamba kifo chake kimeacha pigo katika medani za kisiasa nchini Tanzania. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 22 Julai 2021 na Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma ACT-Wazalendo, Janeth Rithe.

Saa kadhaa baada ya mwanasiasa huyo kufariki dunia, katika Hospitali ya Mount Meru, jijini Arusha, alipokuwa anapatiwa matibabu.

“Taifa limempoteza kiongozi mwenye upeo na uwezo mkubwa wa masuala mbalimbali. Pamoja na kwamba hakuwa mwanachama wala kiongozi, katika chama chetu mpaka umauti unamkuta, historia yake kwetu iliacha alama zisizofutika,” imesema taarifa ya Rithe.

Mghwira alikuwa mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, kuanzia 2015 hadi 2017, alipojiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), tarehe 8 Disemba 2017, baada ya kuteuliwa na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Magufuli, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Hayati Magufuli alipomwapisha Anna Mghwira kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro

Rais Magufuli aliyefariki dunia akiwa madarakani tarehe 17 Machi 2021, alimteua Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, mwezi Juni 2017, akimtoa katika chama cha ACT-Wazalendo, alikokuwa mwenyekiti.

Taarifa ya Rithe imesema, ACT-Wazalendo itautambua na kuuenzi mchango wake, alioutoa kupitia uongozi wake akiwa mwenyekiti wa chama hicho.

“Mama Mghwira alikuwa Mwenyekiti wa kwanza wa ACT Wazalendo, mara baada ya chama kupata usajili wa kudumu kuanzia mwaka 2015 hadi 2017. Chama kitautambua mchango na uongozi alioutoa akiwa mwenyekiti,”imesema taarifa ya Rithe.

Mbali ya kuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Mghwira alikuwa mgombea wa chama hicho katika nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!