Saturday , 10 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo: Mghwira ameacha historia
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo: Mghwira ameacha historia

Anna Mghwira, Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimemlilia aliyekuwa mwenyekiti wake wa kwanza, Anna Mghwira, kikisema kwamba kifo chake kimeacha pigo katika medani za kisiasa nchini Tanzania. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 22 Julai 2021 na Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma ACT-Wazalendo, Janeth Rithe.

Saa kadhaa baada ya mwanasiasa huyo kufariki dunia, katika Hospitali ya Mount Meru, jijini Arusha, alipokuwa anapatiwa matibabu.

“Taifa limempoteza kiongozi mwenye upeo na uwezo mkubwa wa masuala mbalimbali. Pamoja na kwamba hakuwa mwanachama wala kiongozi, katika chama chetu mpaka umauti unamkuta, historia yake kwetu iliacha alama zisizofutika,” imesema taarifa ya Rithe.

Mghwira alikuwa mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, kuanzia 2015 hadi 2017, alipojiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), tarehe 8 Disemba 2017, baada ya kuteuliwa na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Magufuli, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Hayati Magufuli alipomwapisha Anna Mghwira kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro

Rais Magufuli aliyefariki dunia akiwa madarakani tarehe 17 Machi 2021, alimteua Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, mwezi Juni 2017, akimtoa katika chama cha ACT-Wazalendo, alikokuwa mwenyekiti.

Taarifa ya Rithe imesema, ACT-Wazalendo itautambua na kuuenzi mchango wake, alioutoa kupitia uongozi wake akiwa mwenyekiti wa chama hicho.

“Mama Mghwira alikuwa Mwenyekiti wa kwanza wa ACT Wazalendo, mara baada ya chama kupata usajili wa kudumu kuanzia mwaka 2015 hadi 2017. Chama kitautambua mchango na uongozi alioutoa akiwa mwenyekiti,”imesema taarifa ya Rithe.

Mbali ya kuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Mghwira alikuwa mgombea wa chama hicho katika nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!