Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT Wazalendo kumjadili mgombea EALA, uchaguzi mkuu
Habari za Siasa

ACT Wazalendo kumjadili mgombea EALA, uchaguzi mkuu

Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo kinatarajia kufanya kikao cha Halmashauri Kuu tarehe 4 Septemba mwaka huu ambapo pamoja na mambo mengine kitaidhinisha jina la Mgombea wa Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA). Anaripoti Felister Mwaipeta, TUDARCo … (endelea).

Pia kikao hicho kitakachohudhuriwa na viongozi mbalimbali, kitajadili mkakati wa chama hicho kuelekea Uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika mwaka 2024 pamoja na uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Hayo yameelezwa katika taarifa iliyotolewa leo tarehe 30 Agosti, 2022 na Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma ya chama hicho, Janeth Rithe.

Rithe alisema kikao hicho kikitanguliwa na vikao vya siku mbili vya Kamati kuu utakaofanyika tarehe mbili na tatu Septemba jijini Dar es Salaam.

“Kikao cha Halmashauri Kuu kitajadili ujenzi wa chama kuelekea Uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 na Uchaguzi mkuu wa 2025 hasa ikizingatiwa tumejipanga kikimilifu kuelekea uchaguzi huo,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!