CHAMA cha ACT-Wazalendo kimeeleza kuwa uchambuzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) juu ya ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kimepotosha na kimewaahaada watanzania juu ya upotevu wa Sh. 1.5 trilioni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Katibu Itikadi na Uenezi, Ado Shaibu amesema msimamo CCM ndio msimamo wa serikali kutokana na kuwa hicho ndicho chama tawala.
Shaibu ameeleza kuwa CCM miaka ya nyuma kilikuwa na kazi ya kuwafichua mawaziri mizigo lakini sasa kimekuwa kikisikia ripoti kama hizi kimekuwa kikumbatia maovu yanayotendwa na serikali.
Akitoa hoja tano za kukosoa uchambuzi ulifanywa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole.
Shaibu amesema kuwa uchambuzi wa CCM ulikuwa una kejeli na matusi dhidi ya ACT-Wazalendo, ambapo hoja dhaifu ya kuwa ni chama kidogo hakiwezi kufanya uchambuzi.
“Uchambuzi wa Ripoti ya CAG ni suala la kitalaamu halihitaji ukubwa wa chama Uchambuzi wa Ripoti hiyo unahitaji Weledi, Ujuzi na Uzoefu na sivyo kama ilivyoelezwa na Polepole,” amesema Shaibu.
Amesema kuwa Polepole amedanganya kuwa ukaguzi wa CAG ulihusu fedha zilizokusanywa na siyo mapato yaa fedha ghafi na sio fedha tarajiwa.
“CAG ameonesha kuwa Serikali ilikusanya Sh. 25.3 trilioni na kushindwa kukusanya Sh. 4.2 trilioni sawa na asilimia 14.33 ya bajeti yote ya mwaka 2016\2017.”
Shaibu amesema kuwa hakuna pesa ya Zanzibar kwenye ripoti ya CAG na kwamba ingekuwa ingeripotiwa hivyo huo ni upotoshaji kwa umma.
Leave a comment