Spread the love
ABOUD Jumbe Mwinyi, aliyewahi kuwa Rais wa Zanzibar amefariki dunia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu, anaandika Hamisi Mguta.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa kiongozi huyo aliyewahi kuwa mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, amefariki kutokana na maradhi yaliyokua yakimsumbua kwa muda mrefu hadi kufariki kwake.
Jumbe, aliwahi kuwa rais wa Zanzibar mwaka 1972-1984 na aliwahi kushika nafasi mbalimbali ikiwemo Makamu mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi.
More Stories
Takukuru yavimbia wakandarasi, ‘yarejesha’ mil 420 Tanesco
IGP Sirro: Hatufungui kesi za madai, migogoro ya ardhi
Panyabuku waanza kubaini TB