Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa A-Z milipuko ya bomu Uganda, sita wapoteza maisha, 33 wajeruhiwa
Kimataifa

A-Z milipuko ya bomu Uganda, sita wapoteza maisha, 33 wajeruhiwa

Spread the love

 

JUMLA ya watu sita wameripotiwa kupoteza maisha nchini Uganda na wengine 33 kujeruhiwa vibaya kutokana na milipuko ya bomu iliyotokea leo asubuhi tarehe 16 Novemba, 2021 katikati mwa jiji la Kampala nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Polisi nchini humo wamesema milipuko hiyo miwili imetokea katika kituo cha ukaguzi cha polisi karibu na Kituo Kikuu cha polisi wakati mlipuko wa pili ukitokea karibu na geti la kuingia katika Bunge la nchi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini humo, Msemaji wa Polisi- Kamishna Fred Enanga amesema kwa mujibu wa kamera za CCTV, kati ya watu hao sita, watatu ndio waliokuwa wamebeba mabomu hayo na ndiyo waliojitoa mhanga na kufariki papo hapo.

Akizungumzia kuhusu majeruhi, Enanga amesema kati ya majeruhi hao 33, watano wako katika hali ya mahtuti na wengine 17 wamepelekwa katika hospitali mbalimbali nchini humo.

”Mlipuko wa kwanza ulitokea karibu na Kituo Kikuu cha Polisi jiji Kampala muda wa saa 10:03 asubuhi. Picha za kamera za CCTV zimeonesha mwanaume mmoja wa makamo aliyekuwa amevalia koti jeusi na begi mgongoni, alijilipua na kufariki papo hapo.

“Mlipuko huo umejeruhi polisi na raia wengine kutokana na waliokuwa umbali wa mita 30. Wengine wawili walithibitishwa kufariki wakati waliponea chupuchupu lakini wakiwa na majeraha mabaya,” amesema.

Aidha, amesema katika mlipuko wa pili ambao umetoka karibu na Bunge la nchi hiyo, umesabishwa na madareva bodaboda wawili waliojitoa mhanga.

Katika tukio hilo, raia mmoja amefariki papo hapo eneo ambalo pia lipo karibu na majengo makubwa ya Raj na Jubilee Insurance.

Amesema mshukiwa wanne, amekamatwa katika mtaa wa Bwaise jijini humo baada ya kupigwa risasi na polisi kisha kushindwa kujilipua kwa kujitoa mhanga.

Amesema mlipuko huo ambao umetokea ndani ya dakika tatu, saa 10:03 na 10: 06 asubuhi unahusishwa kikundi cha waasi cha Allied Democratic Forces (ADF).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

error: Content is protected !!