Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa 727 wakutwa na corona Kenya, vifo vyafikia 364
Kimataifa

727 wakutwa na corona Kenya, vifo vyafikia 364

Mutahi Kagwe, Waziri wa Afya Kenya 
Spread the love

SERIKALI ya Kenya, imetangaza wagonjwa wapya 727 wa virusi vya corona (COVID-19) baada ya kupima sampuli 6,371 ndani ya saa 24 zilizopita. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kenya imekuwa na utaratibu wa kutoa taarifa za COVID-19 kila siku na leo Jumamosi tarehe 1 Agosti 2020, Waziri wa Afya nchi humo, Mutahi Kagwe amesema, maambukizo yamefikia 21,363.

Amesema, wagonjwa 23 wamefariki dunia akiwemo mtoto wa miaka 16 hivyo kufanya idadi ya waliopoteza maisha kutokana na ugonjwa huo kufikia 364.

Kagwe amesema, kati ya wagonjwa hao wapya, 696 ni Wakenya na 31 ni raia wa kigeni ambapo 465 ni wanaume na 262 ni wanawake.

Waziri huyo amesema, Jiji la Nairobi limeendelea kuwa na maambukizo makubwa kati ya wagonjwa hao wapya, 470 wanatoka jijini humo.

Amebainisha maeneo wanayotoka wagonjwa hao ndani ya Jiji la Nairobi kuwa ni Kiambu (64), Kajiado (25), Kirinyaga (20), Mombasa (16), Migori (15), Busia (13), Machakos (12) na Laikipia wagonjwa 11.

Waziri huyo amesema, wagonjwa 254 wamepona corona ndani ya saa 24 zilizopita na kufanya idadi ya waliopona kufikia 8,419.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!