Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko 69 mbaroni Dar kwa tuhuma za ujangili, wizi mtandao
Habari Mchanganyiko

69 mbaroni Dar kwa tuhuma za ujangili, wizi mtandao

Kamanda Polisi wa Kanda ya Dar es Salaam, Jumanne Murilo
Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limewakamata watu 69 wanaotuhumiwa kwa makosa mbalimbali, ikiwemo kukutwa na nyara za Serikali na wizi wa mtandao. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatano, tarehe 9 Machi 2022 na Kamanda wa Jeshi la Polisi wa kanda hiyo, ACP Jumanne Muliro, akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Kamanda Muliro amesema watuhumiwa hao wamekamatwa kupitia operesheni maalumu ya kuzuia na kuwakamata wahalifu, iliyofanyika kuanzia tarehe 25 Februari hadi 9 Machi 2022.

Amesema, Jeshi la Polisi kushirikiana na Kikosi Kazi cha Kuzuia na Kupambana na Ujangili, limewakamata watuhumiwa watatu, akiwemo Gabriel Mgana na Haffarman Yona, kwa tuhuma za kukamatwa na vipande 25 vya meno ya Tembo.

“Walikamatwa wakiwa na meno ya tembo 25 sawa na tembo 14 waliouawa. Vipande hivyo vyenye uzito wa Kg. 20 vilifichwa ndani ya nyumba ya mmoja wa watuhumiwa hao. Pia gari aina ya Toyota Wiills iliyodaiwa kutumika kusafirisha meno hayo hapa Dar es Salaam, imekamatwa,” amesema Kamanda Muliro.

Wakati huo huo, Kamanda Muliro amesema, Jeshi la polisi limemkamata Khatib Abdala, mkazi wa Banana Kitunda, jijini humo na wenzake watatu, kwa tuhuma za wizi kwa njia ya mtandao kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji hilo.

“Upekuzi wa kina ulifanyika katika nyumba za watuhumiwa hao na walikutwa na jumla ya kadi za simu 46 za kampuni tofauti tofauti, vizibao vinne vya uwakala, simu za mkononi 14 na vitambulisho vitatu vyenye majina yasiyo yao, wanavyotumia katika kazi za kusajili laini hatimaye kuwaibia wateja,” amesema Kamanda Muliro.

Katika matukio mengine, Kamanda Muliro amesema Polisi wamewakamata watu 17, kwa kosa la kupatikana na bhangi kiasi cha masunduku ya chuma mawili, nusu gunia na kete 1,305.

Pia, Kamanda Muliro amesema Polisi imewakamata watu wawili kwa tuhuma za kupatikana na mitambo minne ya kutengenezea pombe ya moshi ‘gongo, lita 780.

1 Comment

  • Wahalifu pale kona ya Morocco-Mwananyamala. Alama inayokataza kuelekea kulia ipo upande wa kushoto wa barabara ya Morocco ukitokea Kimondoni.
    Madereva wengi hawawezi kuiona. Imewekwa kimakosa.
    Lakini, kuna watu bila sare wanafukuza magari kwa pikipiki binafsi na kutishia bosi yuko kwenye simu faini millioni moja …wanadai hongo. Wakipewa wanawaachia.
    Kama kweli hao watu ni Polisi hawatoi vitambulisho halal vinavyotaja cheo,jina na namba. Hivyo, naomba jeshi la polisi lishafishe tabia chafu pale…
    Na vibao viwekwe kulia…na siyo kushoto ili dereva avione kwa urahisi.
    Tumieni alama za barabarani na siyo maneno ya kienyeji.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!