Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Baraza la Mawaziri Tanzania: Majaliwa mguu ndani, nje
Habari za Siasa

Baraza la Mawaziri Tanzania: Majaliwa mguu ndani, nje

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania
Spread the love

 

HOMA imeanza kupanda kwa baadhi ya mawaziri, naibu mawaziri na wabunge, kutokana na kauli ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuwa atafanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Miongoni mwa wanaoelezwa kuwa homa imeanza kuwapanda na kuwashuka, kuwa ni pamoja na Waziri Mkuu wa sasa, Kassim Majaliwa, ambaye naye hajajua hatima yake.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya Serikali na kwa watu wa karibu na Rais Samia, Amiri Jeshi Mkuu huyo wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, anatarajia kufanya mabadiliko hayo, mwanzoni mwa Februari 2022.

Hatua hiyo, inazidisha homa kwa nafasi ya Majaliwa kuendelea ama kuenguliwa kwenye wadhifa huo, alioanza kuutumikia Novemba 20, 2015, alipoapishwa na Rais John Magufuli.

Undani wa habari hii, soma Gazeti la Raia Mwema leo Ijumaa 7 Januari 2022, kujua sura hizo mpya na maoni ya mchambuzi wa masuala ya kisiasa akizungumzia mabadiliko hayo na uchaguzi 2025 unavyoathiriwa na kifo cha aliyekuwa Rais, John Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!