Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtanzania ashinda Tuzo ya Nobel katika fasihi, abeba bilioni 2.6
Habari Mchanganyiko

Mtanzania ashinda Tuzo ya Nobel katika fasihi, abeba bilioni 2.6

Spread the love

 

MWANDISHI wa riwaya nchini Tanzania Abdulrazak Gurnah ametuzwa tuzo ya amani ya Nobel katika fasihi 2021 kutokana na kuangazia suala la ukoloni na athari zake katika utunzi wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Profesa huyo wa fasihi ametangazwa mshindi leo tarehe 7 Oktoba 2021 na Kituo hicho kinachotoa tuzo hizo za Nobel.

Tuzo hiyo inayotolewa na kituo hicho cha Sweden ina thamani ya corona milioni 10 za taifa hilo sawa na Sh bilioni 2.6.

Gurnah mwenye umri wa miaka 73 ni mwandishi wa riwaya 10, ikiwemo Paradise and Desertion.

Riwaya ya Paradise iliyochapishwa 1994, inaangazia hadithi ya mvulana aliyekulia nchini Tanzania katika karne ya 20 na kushinda tuzo ya Booker na kuanza kung’ara katika uandishi wa riwaya.

Yeye ni wa tano kwa jumla, baada ya Wole Soyinka wa Nigeria mwaka 1986, Naguib Mahfouz wa Misri, ambaye alishinda mwaka 1988; na washindi wa Afrika Kusini, Nadine Gordimer mwaka 1991 na John Maxwell Coetzee mwaka 2003.

ABDULRAZAK GURNAH NI NANI?

Licha ya kwamba si maarufu sana Tanzania na Zanzibar, lakini jina lake ni maarufu zaidi duniani.

Umaarufu huo haukutokana tu kwa kuwa Gurnah bali kutokana na umahiri wake katika lugha ya kiengereza na utunzi wa vitabu, Gurnah kwa hivi sasa ni Profesa wa lugha anafundisha katika chuo kikuu cha Kent kilichopo London Uengereza.

Gurnah alizaliwa Visiwani Zanzibar miaka 73 iliyopita, akiwa na umri wa miaka 17 alikimbia Zanzibar nna kuelekea Uengereza kwa lengo la kujiendeleza.

Aliondoka Zanzibar mwaka 1965 ikiwa ni mwaka mmoja tu baada ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 na mwaka mmoja baada ya Muungano wa Zanzibar na iliyokuwa Tanganyika.

Wakati huo fursa za kielimu zilikuwa haba kutokana na kuwepo kwa chuo kikuu kimoja tu maarufu Afrika Mashariki cha Makerere.

Baada ya kuondoka Tanzania alikumbana na changamoto mbalimbali ikiwamo ubaguzi nchini Uingereza. Akiwa hapo Uingereza licha ya changamoto hizo aliamua kujiendeleza hadi kuwa Profesa.

Umaarufu wake hautokani ukimbizi bali unatokana na uwezo wake na tuzo anazopata za utungaji wa vitabu bora ulimwenguni.

Akiwa nchini humo alioa mzungu ambaye anaendelea kuishi naye hadi sasa.

Gurnah baada ya safari yake ndefu ya ukimbizi kwa mara ya kwanza alirejea Zanzibar kutembea akiwa na umri wa miaka 32 mwaka 1980.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!