Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya 52% ya Watanzania wamepima Ukimwi
Afya

52% ya Watanzania wamepima Ukimwi

Spread the love

SERIKALI imesema kuwa Watanzania wapatao 2,405,296 hadi kufikia tarehe Oktoba 2018 walipima VVU kupitia Kampeni ya ‘Furaha Yangu’ ambao ni sawa na asilimia 52 ya lengo la kuwapima watanzania wapatao 4,638,639 hadi Desemba 2018. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Faustine Ndugulile katika kikao cha kamati ya bunge ya huduma za jamii kilichofanyika leo jijini Dodoma.

“Hadi kufikia tarehe 31 Oktoba 2018, jumla ya watanzania 2,405,296 walikuwa wamepima VVU kupitia Kampeni ya ‘Furaha Yangu’ ambao ni sawa na asilimia 52 ya lengo la kuwapima watanzania wapatao 4,638,639 hadi Desemba 2018,” alisema Dk. Ndugulile.

Dk. Ndugulile aliendelea kusema kuwa Miongoni mwa wote waliopima, wanaume walikuwa ni asilimia 44 huku wanawake wakiwa ni asilimia 56. Kati yao, watu 70,436 (2.9%) walikutwa na maambukizi ya VVU, ambapo wanaume 27,984 (2.6%) na wanawake ni 42,452 (3.2%).

Aidha, Dk. Ndugulile alisema kuwa Wizara kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeandaa mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya UKIMWI namba 28 ya mwaka 2008 ili kupendekeza marekebisho yatayoruhusu upimaji Binafsi wa VVU (HIV Self-testing).

Mbali na hayo Dk. Ndugulile alisema kuwa Serikali ipo katika mchakato wa kupunguza umri ya kupima VVU kwa ridhaa ya mzazi au mlezi kutoka miaka 18 hadi 15, hii ni kutokana na kasi ya maambukizi kuongezeka katika umri huo.

Pia, aliendelea kusema kuwa Wizara imeendelea kutoa huduma za Tohara ya kitabibu kwa Wanaume kwa lengo la kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mwanamke kwenda kwa mwanaume katika mikoa ya kipaumbele ambayo haina utamaduni wa kutahiri na ina kiwango kikubwa cha maambukizi ya VVU.

“Hadi kufikia Septemba, 2018 Mikoa kumi na saba (17) inatoa huduma za Tohara ambayo ni Iringa, Njombe, Tabora, Mbeya, Songwe, Rukwa, Katavi, Ruvuma, Shinyanga, Simiyu, Mwanza, Geita, Kagera, Singida, Kigoma, Mara na Morogoro,” alisema Dk. Ndugulile

Aidha, Dk. Ndugulile alisema kuwa Serikali inaendelea kutoa Huduma ya tohara kwa wanaume bila malipo katika vituo vya huduma za afya na kupitia huduma mkoba ngazi ya jamii ambapo hadi kufikia Septemba 2018, jumla ya watu 3,702,387 wamefanyiwa tohara nchini ambao ni wanaume, vijana na watoto wa kiume.

Mbali na hayo Dk. Ndugulile alisema kuwa hadi kufikia mwisho wa Desemba 2018, Wizara iliweza kuwaandikisha katika huduma za tiba na matunzo watu wanaoishi na VVU wapatao 1, 087,382.

Amesema watu 68,927 waliandikishwa katika kipindi cha robo ya mwaka cha Juai hadi Septemba 2018 ambapo kati yao, 1,068,282 wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU, ambapo watoto walikuwa ni 58,908.

Idadi ya vituo vinavyotoa huduma na matunzo vimeongezeka hadi kufikia 6,206 Desemba 2018. Sawa na asilimia 72.7 ya vituo vyote vya huduma za afya nchini.

Miongoni mwa vituo hivyo, vituo kamili vinavyotoa huduma za tiba na matunzo ni 2,103 wakati vituo vinavyotoa huduma ya afya mama na mtoto (RCH) ni 4,103.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!