Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Chama tishio Afrika
Michezo

Chama tishio Afrika

Clatous Chama
Spread the love

 

KIUNGO wa klabu ya Simba, Clatous Chama amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa wiki barani Afrika mara baada ya kuwashinda, Ricardo Goss wa Mamelodi Sundown, Amir Sayoud wa CR Belouizdad na Ferjani Sassi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Chama aliingia kwenye kinyang’anyiro hiko mara baada ya kuonyesha kiwango kizuri kwenye mchezo wa raundi ya tano ya hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya As Vita kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Katika mchezo huo klabu ya Simba, ilifanikiwa kuchomoka na ushindi wa mabao 4-1, hivyo kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kwa mara ya pili katika kipindi cha misimu mitatu ya Ligi.

Katika ushindi huo Chama alifanikiwa kupachika mabao mawili na kutoa pasi moja ya goli (Assist).

Kabla ya kinyang’anyiro hiko cha kupigiwa kura kufungwa, Chama alikuwa akiongoza kwa asilimia 51.

Licha ya kushinda tuzo hiyo, kiungo huyo amechaguliwa kuingia kwenye kikosi bora cha wiki cha Ligi ya Mabingwa barani Afrika.

Hii ni mara ya pili kwa Simba kutoa mchezaji bora wa wiki mara baada ya Luis Miquisone kuchaguliwa katika mzunguko wa pili wa hatua ya makundi ya Ligi ya mabingwa barani Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!