Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo 40 kuingia kambini kuivaa Senegal
Michezo

40 kuingia kambini kuivaa Senegal

Spread the love

JUMLA ya wachezaji 40 wa kikosi cha timu ya Taifa ya Wanawake chini ya umri wa miaka 20, Tanzanite Queen kinatarajia kuingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kufuzu kwa fainali za kombe la dunia dhidi ya Senegal. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kikosi hiko kinatarajia kuingia kambini tarehe 22 Septemba, 2020 hadi 5 Oktoba, huku kikiwa na wachezaji wanaotoka kwenye klabu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake.

Timu hiyo ambayo kwa sasa ipo chini ya kocha Bakari Shime imefanikiwa kufika hatua hii mara baada ya kuitoa timu ya Taifa ya Uganda kwa mabao 4-2 katika mchezo uliofanyika 1 Februari 2020 kwenye Uwanja wa Star Times mjini Kampala.

Senegal itacheza na Tanzania mara baada ya kufanikiwa kuitoa timu ya Taifa ya Sierra Leone kwenye hatua ya awali.

Michuanio hiyo inatarajia kufanyika nchini Costa Rica kuanzia 20 Januari, 2021 hadi 6 Februari 2021.

Majina kamaili ya wachezaji walioitwa kwenye kikosi hiko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!