JUMLA ya wachezaji 40 wa kikosi cha timu ya Taifa ya Wanawake chini ya umri wa miaka 20, Tanzanite Queen kinatarajia kuingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kufuzu kwa fainali za kombe la dunia dhidi ya Senegal. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Kikosi hiko kinatarajia kuingia kambini tarehe 22 Septemba, 2020 hadi 5 Oktoba, huku kikiwa na wachezaji wanaotoka kwenye klabu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake.
Timu hiyo ambayo kwa sasa ipo chini ya kocha Bakari Shime imefanikiwa kufika hatua hii mara baada ya kuitoa timu ya Taifa ya Uganda kwa mabao 4-2 katika mchezo uliofanyika 1 Februari 2020 kwenye Uwanja wa Star Times mjini Kampala.
Senegal itacheza na Tanzania mara baada ya kufanikiwa kuitoa timu ya Taifa ya Sierra Leone kwenye hatua ya awali.
Michuanio hiyo inatarajia kufanyika nchini Costa Rica kuanzia 20 Januari, 2021 hadi 6 Februari 2021.
Majina kamaili ya wachezaji walioitwa kwenye kikosi hiko.
Leave a comment