Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Michezo 40 kuingia kambini kuivaa Senegal
Michezo

40 kuingia kambini kuivaa Senegal

Spread the love

JUMLA ya wachezaji 40 wa kikosi cha timu ya Taifa ya Wanawake chini ya umri wa miaka 20, Tanzanite Queen kinatarajia kuingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kufuzu kwa fainali za kombe la dunia dhidi ya Senegal. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kikosi hiko kinatarajia kuingia kambini tarehe 22 Septemba, 2020 hadi 5 Oktoba, huku kikiwa na wachezaji wanaotoka kwenye klabu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake.

Timu hiyo ambayo kwa sasa ipo chini ya kocha Bakari Shime imefanikiwa kufika hatua hii mara baada ya kuitoa timu ya Taifa ya Uganda kwa mabao 4-2 katika mchezo uliofanyika 1 Februari 2020 kwenye Uwanja wa Star Times mjini Kampala.

Senegal itacheza na Tanzania mara baada ya kufanikiwa kuitoa timu ya Taifa ya Sierra Leone kwenye hatua ya awali.

Michuanio hiyo inatarajia kufanyika nchini Costa Rica kuanzia 20 Januari, 2021 hadi 6 Februari 2021.

Majina kamaili ya wachezaji walioitwa kwenye kikosi hiko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

Michezo

Mwenyekiti UVCCM anogesha nusu fainali Kimwanga CUP, Hawa Abdul Rede CUP kwa kishindo

Spread the loveHEKAHEKA za michuano ya kuwania kuingia fainali ya michuano ya...

Michezo

Yanga SC. yatwaa ubingwa wa pili mfululizo

Spread the love  KLABU ya Yanga SC imeweka rekodi ya kutwaa ubingwa...

error: Content is protected !!