Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Marekani yamkana Lissu, JPM
Habari za SiasaTangulizi

Marekani yamkana Lissu, JPM

Spread the love

LICHA ya Dk. John Magufuli, mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM na Tundu Lissu, mgombea urais kupitia Chadema kutawala siasa ngazi ya urais, Marekani imeeleza kutounga mkono mgombea wala chama chochote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Na kwamba, inaunga mkono kwa karibu mchakato wa demokrasia unavyoweza kushika hatamu kwenye uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

Kwenye taarifa yake iliyotolewa tarehe 1 Oktoba 2020 kupitia ubalozi wake nchini hapa, Marekani imeeleza inaunga mkono haki na uhuru kabla, wakati na baada ya uchaguzi huo.

Taarifa hiyo imeeleza, Marekani na mataifa mengine wanafuatilia kwa karibu matendo ya watu wanaoingilia na kuvuruga mchakato wa kidemokrasia au kuchochea vurugu dhidi ya raia kabla, wakati au baada ya uchaguzi.

Taifa hilo limeeleza, linaunga mkono wito uliotolewa na wagombea wakuu kwa kuwapo mchakato wa uchaguzi wa amani na wenye uwazi.

“Tunatoa wito kwao na kwa wafuasi wao kuchukua hatua kutanzua hali ya uhasama inayojengeka na kuepuka matamshi ya kichochezi,” imeeza taarifa hiyo na kuongeza:

“Hatutasita kufikiria kuchukua hatua stahiki kwa wale watakaobainika kuhusika katika vurugu na machafuko yanayohusiana na uchaguzi au kukwaza mchakato wa kidemokrasia.”

taarifa hiyo imefafanua kwamba, uendeshaji wa uchaguzi mwingine nchini utakuwa na matokeo muhimu si kwa Tanzania yenyewe pekee, bali pia kwa kanda nzima ya Afrika Mashariki.

Pia taarifa hiyo imeeleza, historia ya Tanzania ya kuendesha chaguzi zinazohusisha vyama vingi, inarudi nyuma hadi miaka 25 iliyopita na kuifanya Tanzania kuwa mfano wa kuigwa Afrika.

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!