KAMATI ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) 2019/20, imetoa orodha ya majina 30 ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa ligi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Ligi hiyo iliyokuwa na timu 20, imehitimishwa hivi karibuni huku bingwa akiwa timu ya Simba SC ya jijini Dar es Salaam iliyotwaa kombe hilo mara tatu mfululizo.
Pia, imeshuhudia timu za Singida United, Lupuli ya Iringa, Alliance ya Mwanza na Ndanda ya Mtwara zikishuka daraja.
Kati ya orodha hiyo ya wachezaji 30, Simba imeingiza wachezaji nane huku Yanga ya Dar es Salaam ikiwa na wachezaji watano na Azam FC ya jijini humo wachezaji watatu.
Taarifa kamili ya kamati hiyo iliyotolewa leo Ijumaa tarehe 31 Julai 2020 hii hapa;
Leave a comment