Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Watumishi wa Jiji la Dodoma watakiwa kushiriki usafi
Habari Mchanganyiko

Watumishi wa Jiji la Dodoma watakiwa kushiriki usafi

Dickson Kimaro, Mkuu wa Idara ya Mazingira na Mdhibiti wa Taka ngumu wa Jiji la Dodoma
Spread the love

WATUMISHI wa taasisi mbalimbali za serikali wametakiwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la usafi ambalo ufanyika kila jumamosi kuanzia saa moja kamili hadi saa tatu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hamasa hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Idara ya Mazingira na Mthibiti wa Taka ngumu katika Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro muda mfupi baada ya kumalizika kwa zoezi la usafi.

Kimaro amesema kuwa watumishi wa serikali wamekuwa changamoto kubwa katika kushiriki shughuli za usafi licha ya kuwa ni jambo ambalo linafahamika.

Aidha amesema zoezi la usafi limekuwa likifanywa kila jumamosi ukiachilia jumamosi ya mwisho wa mwezi ambapo usafi ufanywa kwa kumuunga mkono Makamu wa Rais.

“Unaweza kuona hapa waliowengi ni akina mama na vijana lakini watumishi wa wengi wa serikali hawapo.

“Sisi watumishi wa umma tunatakiwa kuonesha mfano ndipo tutakuwa na ujasiri wa kuwahimiza wananchi kufanya usafi na kutii sheria pasipo shuruti,” amesema Kimaro.

Akizungumzia umuhimu wa kufanya usafi katika Jiji la Dodoma amesema kuwa ni kulifanya jiji kuwa la tofauti na lilivyokuwa Manispaa kwa lengo la kulifanya kuwa na mvuto wa aina yake.

“Licha ya Dodoma kuwa Jiji bado ni makao makuu hivyo ni wajibu wa kila Mwananchi mkazi wa Dodoma na ambaye siyo mkazi kuhakikisha anatunza mazingira na kulifanya jiji kuwa safi muda wote.

“Jambo lingine ni kupambana na magonjwa ya mlipuko ambayo yanaweza kujitokeza kama hapatakuwepo na usafi wa kutosha hasa magonjwa ya kuhara na mazalia ya mbu ambayo yanaweza kusababisha maralia au Dengue,” amesema Kimaro.

Mbali na hivyo amesema kuwa kwa sasa katika jiji la Dodoma hakuna changamoto ya ukosefu wa vyoo bora hata hivyo ameeleza kuwa bado kero ya ukosefu wa hupo maeneo ambayo bado hayajapimwa na wananchi kurasimishwa.

Pamoja na hayo Kimaro ameitaka jamii kuhakikisha inajenga vyoo bora na kushiriki kikamilifu katika utunzani wa mazingira kuanzia majumbani wanamoishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!