Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa 25 wafariki dunia katika shambulizi Ukraine
Kimataifa

25 wafariki dunia katika shambulizi Ukraine

Spread the love

 

RAIS wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy amesema idadi ya vifo kutokana na shambulio la kombora la Urusi kwenye jengo la ghorofa tisa katika mji wa kusini mashariki mwa Ukraine wa Dnipro imefikia 25. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Amesema hayo wakati waokoaji wakijaribu kuwaondoa manusura zaidi kutoka kwenye mabaki hayo.

Waokozi walitumia vifaa maalumu kujaribu kuwafikia watu waliokwama kwenye ghorofa za juu za jengo hilo lenye wakazi 1,700, ambao baadhi yao walitoa ishara ya kuomba msaada kwa taa za simu zao za mkononi.

Shughuli za utafutaji na uokoaji ziliendelea mpaka nyakati za mchana. Rais Zelenskyy aliahidi kupigania kila maisha ya watu waliokumbwa na shambulizi hilo.

Pia alisema watu 73 walijeruhiwa katika shambulio hilo juzi tarehe 14 Januari, 2023 huku 39 wakiokolewa jana alasiri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!