RAIS wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy amesema idadi ya vifo kutokana na shambulio la kombora la Urusi kwenye jengo la ghorofa tisa katika mji wa kusini mashariki mwa Ukraine wa Dnipro imefikia 25. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Amesema hayo wakati waokoaji wakijaribu kuwaondoa manusura zaidi kutoka kwenye mabaki hayo.
Waokozi walitumia vifaa maalumu kujaribu kuwafikia watu waliokwama kwenye ghorofa za juu za jengo hilo lenye wakazi 1,700, ambao baadhi yao walitoa ishara ya kuomba msaada kwa taa za simu zao za mkononi.
Shughuli za utafutaji na uokoaji ziliendelea mpaka nyakati za mchana. Rais Zelenskyy aliahidi kupigania kila maisha ya watu waliokumbwa na shambulizi hilo.
Pia alisema watu 73 walijeruhiwa katika shambulio hilo juzi tarehe 14 Januari, 2023 huku 39 wakiokolewa jana alasiri.
Leave a comment