Dina Boluarte
BUNGE la Peru limemuondoa madarakani Rais wa nchi hiyo, Dina Boluarte kwa kura nyingi za wabunge, kufuatia hoja za kutokuwa na uwezo wa kudumu wa maadili katika kutekeleza majukumu yake. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Raisi huyo ameondolewa madarakani usiku wa tarehe 9 Oktoba 2025 na kutangazwa na spika wa bunge José Jerí na kusema anaweza kujitetea au kuakilishwa na wakili na kudai kuwa katika kikao hicho rais Boluarte hakufika licha ya kutakiwa kuhudhuria
Kutimuliwa kwa rais kumeidhinishwa, anaweza kujitetea au kuwakilishwa na wakili” ametangaza Spika wa Bunge José Jerí ametolewa madarakani kupitia kura zilizopigwa na wabunge 87 kati ya 122 walioshiriki katika kura hiyo, walilazimika kupiga kura kuunga mkono kuondolewa kwake.
Kabla ya kura hizo vyama vikuu vya kisiasa katika Bunge viliwasilisha hoja tano za kumtimua madarakani wakati wa mchana uchunguzi wa hoja nne kati hizo zilipitishwa kwa kura nyingi katika Bunge la nchi hiyo.
Ikumbuke kuwa rais Boluarte alipata nafasi hiyo kupitia kuondolewa kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Pedro Castillo kutokana na jaribio la kutaka kuvunja bunge mwaka 2022 kipindi hicho rais Boluarte akiwa makamu wake.
ZINAZOFANANA
Mazishi ya kitaifa ya Ali Khamenei yaahirishwa
Ronaldo akimbia vita Saudia, aelekea Madrid
Vigogo hawa wameondoka, katika vita kati ya Marekani na Iran